HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 19, 2013

'BADO MDOGO' YA ASLAY KISA CHA KWELI


Na Elizabeth John


BAADA ya kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘Naenda Kusema kwa mama’, Kinda wa muziki wa kizazi kipya nchini, Asilahi Isihaka Dogo Asley, amefunguka juu ya uhalisia wa wimbo wake mpya wa ‘Bado Mdogo’, liomshirikisha mwanadada Estelina Sanga ‘Lina’.

Wimbo huo ambao unazungumzia mama anaependa kufatilia watoto wadogo na kuwataka kimapenzi, tayari umeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio kutokana na ubora wa mashairi yake.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Dogo Aslay alisema wimbo huo ni kwa ajili ya kuwaelimisha vijana juu ya maswaha hayo, lakini pia ni story ya kweli iliyomtokea yeye akiwa na miaka 16 pale tu alipotoka na ngoma yake ya kwanza ‘Naenda kusema kwa Mama’.

“Mimi nataka tu kuwaambia vijana wenzangu kwamba usiombe yakukute mambo haya wewe yasikie tu kwa watu, huo wimbo ni historia ya kweli na ukimuangalia mama mwenyewe hata mama yangu mzazi hamkuti kiumri,” alisema.


Pia aliwataka wapenzi wa kazi zake kumpa sapoti katika kazi zake zilizopita pamoja na zinazo kuja na kwamba wakae mkao wa kula kwaajili ya kuipokea video ya ngoma hiyo ambayo inafanya vizuri katika chati ya muziki huo.

No comments:

Post a Comment

Pages