HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 23, 2014

Castle Lite yataja wa Timbaland
Meneja Msaidizi wa Bia ya Castle Lite, Geofrey Makau (kulia), akimkabidhi mmoja kati ya washindi wa Promosheni ya Castle Lite,  Ratifu Komba tiketi ya kwenda nchini Afrika ya Kusini kushuhudia Tamasha kubwa la TIMBALAND litakalofanyika nchini humo mwanzoni mwa Mwezi Juni. Kushoto ni Meneja wa Bia ya Castle Lite, Victoria Kimaro. (Picha na Francis Dande)

Na Mwandishi Wetu

KINYWAJI cha Castle Lite kinachozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), jana imetaja majina ya Watanzania 12 watakaoshuhudia ‘live’ onyesho la msanii maarufu duniani, Timothy Zachery Mosley aliye maarufu kwa jina la Timbaland.

Onyesho hilo linatarajiwa kufanyika Johannesburg, Afrika Kusini hapo Juni, mwaka huu, huku watu hao 12 wakilipiwa kila kitu ili kushuhudia mambo makali kutoka kwa msanii huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa Bia ya Castle Lite, Victoria Kimaro alisema, wanajisikia faraja kupata watu hao waliotokana na promosheni iliyoendeshwa nchi nzima.

Katika promosheni hiyo, wateja na wapenzi wa Castle Lite walitakiwa kutuma namba zilizo chini ya kizibo cha bia hiyo na hatimaye washindi kupatikana kupitia droo iliyofanyika.

“Kwetu kama Castle Lite tunawapongeza s wateja hawa 12 ambao wamefanikiwa kuibuka kidedea katika promosheni hii tuliyoizindua Januari na kumalizika Aprili 4.

 “ Kama tulivyoahidi  wakati wa uzinduzi, washindi hawa wataondoka nchini Juni 6, mwaka huu kwenda Afrika Kusini kushuhudia tamasha hilo.

“Washindi wetu watalipiwa gharama zote za usafiri, malazi, chakula na usafiri wa ndani wakiwa huko na mambo yote haya yatafanywa katika kiwango cha hali ya juu, yaani watachukuliwa kama watu maalumu,” alisema.

Aliwataja washindi hao hao na sehemu wanazotoka zikiwa kwenye mabano kuwa ni, Ratifu Gabriel Komba, William Yobu Msangi, Emmanuel Mathayo Mushi na Amandi Mathayo Kimario ambao wote wanatoka Dar es Salaam.

Wengine ni Bryson Evarist Temu, Gabriel Pankrias Liyakurwa (Kilimanjaro), Kolman Julius Shayo (Mwanza), Fidelis Festus Tesha (Dodoma) na Dickson Ladislaub Kanoni (Tabora).

Wapo pia Dorika Stephania Chirigati, John Jackson Ringo na Frank John Zaburi ambao nao pia wanatoka Dar es Salaam.

Victoria, aliwataka washindi hao kuwa mabalozi wazuri wa Castle Lite muda wote na aliwashukuru wote walioshiriki katika promosheni hiyo.

Bia ya Castle Lite inazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL)

No comments:

Post a Comment

Pages