NA
ELIZABETH JOHN
MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb
Abdul ‘Diamond Platinumz’ amewataka Watanzania kuendelea kumpa sapoti katika
kazi zake kwa lengo la kuendelea kuiwakilisha vema tasnia ya muziki katika
mataifa mbalimbali.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana baada ya
kuwasili nchini akitokea Marekani katika utoaji tuzo za AFRIMMA zilizofanyika
usiku wa kuamkia Julai 28.
Diamond alishinda tuzo mbili za msanii bora wa
kiume Afrika Mashariki na wimbo bora wa kushirikiana ambao ni ‘My Number One’
alioimba na mkali kutoka Nigeria, Davido.
Katika mapokezi hayo, Diamond alipokelewa na mamia
ya Watanzania ambapo kila mmoja aliyefika katika uwanja huo alitamani kumpa
mkono wa hongera msanii huyo.
“Naomba sapoti mnayonionesha sasa hivi muendelee
nayo, nashukuru mungu kwa kuniwezesha kufika hapa najua ni kutokana na sapoti
zenu hivyo nawashukuru sana,” alisema Diamond.
Mtanzania mwingine aliyeshinda katika tuzo hizo ni
mwadada Judith Wambura ‘Lady JayDee’ ameshinda msanii bora wa kike wa Afrika
Mashariki na mtayarishaji bora wa muziki huo Afrika Mashariki ni Sheddy Clever.
No comments:
Post a Comment