HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 13, 2014

MH: NAMELOK SOKOINE ATIMIZA AHADI YAKE KWA KIKUNDI CHA VIKOBA- ARUSHA

Mbunge wa viti maalum CCM mkoa wa Arusha, Namelok Sokoine (kushoto), akikabidhi Shs. milioni 5 kwa Mwenyekiti wa Vikoba Kata ya Engutoto, Bilhuda Kisasa,  ikiwa ni sehemu ya mchango wake wa shs. milioni 10 alizoahidi kuwasaidia akinamama wa kata hiyo. (Na Mpiga Picha Wetu)
Mbunge wa viti maalum CCM mkoa wa Arusha, Namelok Sokoine (kulia), akizindua katiba ya vikundi vya vikoba katika kata ya Engutoto Wilayani Monduli jana. Hafla hiyo ilikwenda sambamba na harambee ya kutunisha mfuko wa vikoba, ambapo katika harambee hiyo jumla ya shilingi milioni 12 zilipatikana. Kushoto ni Mwenyekiti wa vikoba kata ya Engutoto, Bilhuda Kisasa .

Mbunge wa viti maalum CCM mkoa wa Arusha, Namelok Sokoine (kulia), akizindua katiba ya vikundi vya vikoba katika kata ya Engutoto Wilayani Monduli jana. Hafla hiyo ilikwenda sambamba na harambee ya kutunisha mfuko wa vikoba, ambapo katika harambee hiyo jumla ya shilingi milioni 12 zilipatikana. Kushoto ni Mwenyekiti wa vikoba kata ya Engutoto, Bilhuda Kisasa. 

NA  MWANDISHI  WETU,  ARUSHA

WANACHAMA wa vikundi vya kuweka na kukopa (VIKOBA) mkoani Arusha wametakiwa kutumia na kupanga vizuri matumizi ya fedha wanazokusanya ili ziwasaidie kutoka daraja mhadi jingine katika maisha yao.



Kauli hiyo ilitolewa wilayani hapa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Arusha Namelok Sokoine alipokuwa akiendesha utunishaji wa fedha kwa Umoja wa Wanavikoba wa Kata ya Engutoto yenye vikundi 20 na wanachama 600.



Katika utunishaji huo, Namelok alichangia Sh. Milioni 10 huku kiasi cha Sh. Milioni 12 kikipatikana katika shughuli hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Umoja wa Wanawake UTW wilayani Monduli.



Akizungumza na wanavikundi hao Mbunge Namelok aliwataka wanawake kujitokeza na kujiunga katika vikundi huku akiwataka kuacha kuogopa kufanya shughuli za ujasiriamali.



“Wanawake nawaomba sana muendelee kujitokeza na kujiunga katika Vikoba kwani huku ndipo eneo ambalo litatuwezesha tuwe na sauti ya kujitegemea kimapato.



“Lakini pia naomba niwakumbushe jambo muhimu hizi fedha tunazokusanya nawaomba sana muonyeshe mfano wa kuzitumia vizuri ili kesho zitusaidie kutoka daraja moja kwenda daraja jingine katika maisha yetu,” alisema Namelok.



Kwa upande wake Katibu wa UWT Kata ya Engutoto Glory Emmanuel alisema wana vikundi wengi waliopo kwenye vikoba wanakabiliwa na changamoto ya elimu ya ujasiriamali.



“Tunaomba suala la ofisi za vikoba uliangalie kwani vikundi havina ofisini.Pia wanachama hawana elimu hatua inayosababisha kukopa na kutumia sivyo kutokana na kutokuwa na elimu ndogo ya biashara,” alisema Glory.



Naye mwana kikundi Zaituni Mwishehe alibainisha jinsi alivyonufaika na kuwa katika vikundi hivyo vya kuweka na kukopa ambapo hadi sasa ameweza kujitegemea katika matumizi ya kawaida ndani ya nyumba.



“Sasa hivi naweza kulipia michango midogomidogo ya mwanangu shuleni. Lakini pia hata kutatua matatizo mengine ya kifamilia kupitia mikopo ninayochukua kwenye kikundi bila hata kumsubiria mume wangu,” alisema Zaituni.

No comments:

Post a Comment

Pages