Shirika la AGPAHI ni
shirika la Kitanzania linalofanya kazi ya kutokomeza UKIMWI na kuzuia maambukizi
mapya ya virusi vya ukimwi (VVU) kwa watoto. AGPAHI ilianzishwa kwa msaada
wa Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation (EGPAF) mwaka 2011kwa lengo
la kutokomeza UKIMWI kwa watoto wachanga nchini Tanzania.
AGPAHI na EGPAF ni mashirika mawili yanayojitegemea na ni washirika kupitia makubaliano baina yao. AGPAHI inafanya kazi kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Tanzania katika kusaidia kutoa huduma za kinga, matunzo na matibabu kwa watu wanaoishi na VVU katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Geita.
Rais na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Elizabeth
Glaser Pediatric AIDS Foundation (EGPAF), Charles Lyons (kushoto), akipata
maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Laurean Bwanakunu wakati
alipotembelea ofisi za shirika hilo
zilizopo Upanga jijini Dar es Salaam, kuangalia maendeleo yake tangu
lianzishwe mwaka 2011. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa EGPAF Tanzania, Jeroen
Van’t Pad Bosch.
Rais na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation (EGPAF), Charles Lyons akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa AGPAHI.
Viongozi wa Shirika la EGPAF wakiwa katika mkutano na baadhi ya wafanyakazi wa AGPAHI.
Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Laurean Bwanakunu akizungumza
wakati wa mkutano na Rais na Mtendaji Mkuu wa Shirika la EGPAF, Charles
Lyons aliyetembelea ofisi za shirika hilo hapa Dar es Salaam.
Bwana,
Charles Lyons (katikati), akishiriki chakula cha mchana na wafanyakazi wa
AGPAHI.
Wafanyakazi wa AGPAHI wakisalimiana na Rais na Mtendaji Mkuu
wa Shirika la EGPAF.
Rais na Mtendaji Mkuu wa Shirika la EGPAF, Bw. Charles Lyons (kushoto) akiondoka katika
ofisi za AGPAHI, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Bw. Laurean Bwanakunu.Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Ufundi wa AGPAHI, Dk. Amos Nsheha na Mkurugenzi wa EGPAF Tanzania, Jeroen Van’t Pad Bosch.
No comments:
Post a Comment