HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 17, 2014

SHEREHE ZA JESHI LA ANGA KUTIMIZA MIAKA 32 KUFANYIKA JIJINI MWANZA JULAI 23-28


Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga Meja Jenerali, Joseph Furaha Kapwani akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sherehe za miaka 32 ya tangu kuanzishwa kwa kamandi hiyo. Kulia ni Mkurugenzi wa Usalama na Utambuzi, Meja Erick Cleiphas. (Picha na Francis Dande)
Waandishi wsa habari wakimzikiliza Mkuu wa  Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga, Meja Jenerali, Joseph Furaha Kapwani.


Na Ramadhani Tembo
 
KAMANDI ya Jeshi la Anga nchi imejipanga kuonyesha zana zake za kivita na majukumu yake katika maadhimisho ya miaka 32 tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1982, yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza Julai 23-28 mwaka huu. 

Maadhimisho hayo yatahudhuriwa na viongozi mbalimbali wanchi,majeshi ya ulinzi na usalama, wananchi wa kanda ya ziwa ,mikoa ya jirani na Taifa kwa ujumla na kupata fursa ya kuona zana mbalimbali za anga zinazotumika na Jeshi hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo, Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga, Meja Jenerali, Joseph Kapwani amesema kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kusherehekea miaka 32 na kujitathmini kiutendaji.

“Tunatarajia kufanya maadhimisho hayo ili wananchi wajue kazi mbalimbali zinazofanywa na jeshi hilo na kuwahamasisha vijana wanaopenda kujiunga na Jeshi la Anga”alisema.

Alisema Kamandi hiyo ni moja kati ya Kamandi tatu zinazounda Jeshi la Ulinzi na Usalama (JWTZ) ambayo inahusika na jukumu la kuhakikisha anga linakuwa salama wakati wote kwa kutumia ndege za kivita,ndege za usafirishaji,makombora,na mizinga ya kudungulia ndege. 

Aliongeza kuwa mpaka sasa Jeshi hilo linamafanikio makubwa na linawahakikishia watanzania hali ya usalama wa anga itakuwa salama wakati wote.

No comments:

Post a Comment

Pages