HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 28, 2014

Askofu Aijia Juu Serikali; asema Katiba isiwe ya Chama Kimoja.

Na Bryceson Mathias, Dodoma
 
MSAIDIZI wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Samwel Mshana, ameijia juu Serikali akisema Mchakato wa kupata Katiba Mpya usiwe wa Chama Kimoja, hivyo wanawake wasilala usingizi wakahukumiwa, maana Yesu anakuja.

Akifungua Tamasha la siku tatu la Wanawake wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Makao Makuu Agosti 28 mwaka, Mshana alinukuu maandiko ya Mathayo 25:1-12 kuhus Wanawali 10, ambapo Watano walikuwa na Busara, Watano Wapumbavu.

“Yesu alisema, ‘Mimi ni Njia Kweli na Uzima’, hivyo Mwanamke mwenye mafuta anayetegemea  Kweli, hawezi kugombana na Ndoa yake, Viongozi wa Kanisa na Serikali, na   hawezi kutaka Katiba ya Chama au Kundi fulani, atataka inayounganisha Vyama na Dini zote.

Wanawake msitumiwe vibaya na Vyama vya Siasa, Makundi yoyote au Mtu binafsi, maana kwa kufanya hivyo mtakuwa mnapoteza heshima na Busara yenu iliyo katika Zaburi 68:11 ‘Bwana analitoa Neno lake, Wanawake watangazao habari ni Jeshi kubwa”.alisema Mshana’.

Wanawake watangazao habari ni Jeshi kubwa ni Kauli Mbiu ya Tamasha hilo la Wanawaka wa KKKT Jimbo la Makao Makuu Dodoma, ambayo itaambatana na Mafundisho ya Maadili ya Mwanamke katika Kanisa, Ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia kwa wakati huu.

Askofu Mshana amelaani Mauaji ya Wanawake na Albino yaliyoshamiri katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Arusha na pengineyo, ambapo amesema Kanisa litaendelea kumuomba Mungu likipinga Watu waovu wanaotaka kutatua mambo yao kwa kutenda vitendo Viovu.

Hata hivyo Mshana ameitaka Serikali kutumia Mamlaka yake kuhakikisha inakomesha mauaji hayo badala ya kuwa na Maneno mengi ya kuwatumainisha Wananchi kwenye Majukwaa ya Kisiasa lakini hawachukui hatua zinazowahakikishia watu Usalama wa Maisha na Mali zao.

No comments:

Post a Comment

Pages