HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 21, 2014

SHEIKH FARID ADAI ALIHOJIWA AKIWA UCHI

 Watuhumiwa wa kesi ya Ugaidi wakiingia katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo.
Wakiingia Mahakamani.
Sheikh Farid akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam huku akiambatana na watuhumiwa wenzake.

WASHITAKIWA 20 wanaokabiliwa na mashtaka mbalimbali ya kigaidi hapa nchini leo wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, huku wakilalamikia kupata mateso wakiwa mahabusu.

Washtakiwa hao wameyasema hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salama, mbele ya Hakimu Mkazi Hellen Liwa, baada ya waendesha mashitaka wa Serikali, Pita Njike  na George Balasa kuiomba mahakama iwaruhusu kuwachukua washitakiwa saba ili waende kuhojiwa kwa upelelezi zaidi.

Washitakiwa walioombwa kwenda kuhojiwa ni Sheikh Farid Hadi Ahmed, Ramadhani Alawi, Amour Juma, Mohamed Yusuph, Nassoro Abdalah, Hamis Amour na Hassani Bakari.

Ndipo mshitakiwa namba moja katika kesi hiyo Sheikh Farid Hadi Ahmed ambaye pia ni kiongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) alisema kuwa mara ya kwanza walipoombwa mahakamani hapo ili kwenda kuhojiwa, hawkufanyiwa ustarabu wala ubinadamu. "tulihojiwa tukiwa uchi" amesema Sheikh Farid.
   
“Watu wameumizwa vibaya hayasemeki, kuna mtu hapa anakojoa damu wiki ya pili sasa lakini hatujapewa matibabu yoyote,kwahiyo muheshimiwa hakimu tunaomba mtutafutie Dactari aje afanye uchunguzi juu ya afya zetu.Vinginevyo muheshimiwa siku utaletewa maiti hapa mahakamani” alisema Farid.

Naye mshitakiwa namba 12 katika kesi hiyo Salum Ali Salum,alidai mbele ya mahakama hiyo kuwa ameingiliwa kinyume na maumbile  kinguvu, na ameimgiziwa chupa na mti sehemu zake za nyuma.

“Nakuomba muheshimiwa Hakimu kama unaweza twende faragha nikakuonyeshe,hapa nilipo sehemu zangu za nyuma zinavuja ,nimeingizwa jiti mpaka limekatikia,kwahiyo muheshimiwa naomba nipatiwe matibabu”alisema Salum.

Hakimu aliwataka washitakiwa walete malalamiko yao kwa njia ya maandishi,washitakiwa wite walirudishwa rumande hadi Septemba 3 mwaka huu.

Wakati huohuo mahakama hiyo imelazimika kuiahilisha kesi inayowakabili viongozi wawili wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) ), Mselem Ally Mselem na Abdallah Said Alli (Madawa),kwasababu mshitakiwa Mselem Ally Mselem hakuweza kufika mahakamani hapo kwakuwa ni mgojwa.

Akiahiahilisha kesi hiyo Hakimu Mkazi Agustino Mbando,Waendesha mashitaka wa serikali Peter Njige na George Balasa,walidai mshitakiwa namba moja hakufika mahakamani ,kwahiyo wakamuomba hakimu apange tarehe nyingine ya kuja kutajwa tena kwa kesi hiyo.

Awali washitakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo wakikabiliwa na mashitaka matatu likiwamo la kuingiza watu kufanya vitendo vya kigaidi nchini.

Hakimu Mbando aliihailisha kesi hiyo mpaka Septemba 3 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Pages