Wanafunzi wa Shule ya Kinyambwiga A na B iliyopo Wilaya ya Bunda Mkoa wa Mara wakiwa wamekaa
kwenye mawe na magogo ya miti kutokana na shule hizo kutokuwa na vyumba vya
madarasa na madawati. (Picha na Ahmed Makongo)
Wanafunzi wa Shule ya Kinyambwiga A na B wakiwa wamekaa
kwenye mawe na magogo ya miti kutokana na shule hizo kutokuwa na vyumba vya
madasa na madawati.
Wanafunzi wa Shule ya Kinyambwiga A na B wakiwa wamekaa
kwenye mawe na magogo ya miti kutokana na shule hizo kutokuwa na vyumba vya
madasa na madawati.
Wanafunzi wa Shule ya Kinyambwiga A na B wakiwa wamekaa
kwenye mawe na magogo ya miti kutokana na shule hizo kutokuwa na vyumba vya
madasa na madawati.
Na Ahmed Makongo, Bunda
WANAFUNZI
zaidi ya 300 wa shule za msingi za Kinyambwiga A na B, zilizoko Katika Wilaya
ya Bunda, Mkoani Mara, wanaosomea nje kwenye miti wakiwa wamekalia mawe na
magogo ya miti, wamesema kuwa wanaathirika sana kiafya na kielimu, kutokana na
kupigwa baridi, kunyeshewa mvua, kuchomwa na jua na kukaa kwenye mavumbi.
Kutokana na kukosa vyumba vya madarasa, ambapo mbao za
kuwafundishia zimepigiliwa kwenye miti, huku wao wakiwa wamekaa kwenye mawe na
kwenye magogo ya miti kwa kukosa madawati, walisema kuwa wanaathirika sana ki-afya
na ki-elimu kutokana na hali hiyo.
Wanafunzi zaidi
ya 130 wanaosomea nje kwenye miti ambayo imegeuzwa kama vyumba vya madarasa ni wa
shule ya msingi Kinyambwiga A, ambao ni wa darasa la pili na tano, waliliambia
gazei hili kuwa wanaathirika sana na hivyo wanaomba kuondolewa kero hiyo, ili
waweze kupata elimu inayostahili kama wanafunzi wengine walioko kwenye shule
zenye ubora.
Nao
wanafunzi wa shule ya msingi Kinyambwiga B ambao ni wa madarasa ya pili, tano
na sita zaidi ya 180, walisema kuwa wao pia wanaathirika na hali hiyo ya
kusomea nje na kukaa kwenye mawe na kwenye magogo ya miti.
Wanafunzi wa
shule hizo zote kwa ujumla walisema kuwa wanaathirika sana kiafya na kielimu
kutokana na mazingira wanayosomea.
Wanafunzi
hao waliwaomba wazazi, wananchi na serikali kwa ujumla, kuwaondolea kero hiyo, Ili
waweze kusomea Katika mazingira yanayofaa ili waweze kupata elimu inayostahili
kama walivyo wanafunzi waosomea kwenye vyumba vya madarasa na kukaa kwenye
madawati.
“Hali hii ya
kusomea nje na kukaa kwenye mawe na magogo ya miti kwa ujumla sisi tunaathirika
sana kielimu na pia kiafya, maana tunapigwa baridi wakati wa asubuhi,
tunanyeshewa mvua wakati zinapokuja, tunachomwa na jua wakiti wa mchana na
tunaathirika kiafya kwa kukaa kwenye ya mavumbi” walipaza sauti zao wanafunzi hao wakati wakizungumza na mwandishi
wa habari hizi.
Baadhi ya
walimu wa shule hizo wakiwemo walimu wakuu, walisema kuwa kutokana na hali hiyo
wamekuwa wakifundisha Katika mazingira magumu, hali ambayo inawafanya watoto
kutokuelewa vyema, ikiwa ni pamoja na kutokuwa na miandiko mizuri.
“Hata
hawafanyi vizuri kwa kutokuandika
vizuri, pia sisi walimu hata hali ya ufundishaji inakuwa Katika mazingira
magumu” alisema mwalimu Mussa Lubeleli wa shule ya msingi Kinyambwiga A.
Afisa elimu
wa shule za msingi katika Wilaya ya Bunda, Jeshi Pembe, alithibitisha wanafunzi
hao kusomea nje kwa sababu ya kutokuwa na vyumba vya madarasa na kukaa kwenye
mawe na kwenye magogo ya miti kwa kukosa madawati.
Pembe
alisema kuwa hali hiyo inasababishwa na wananchi wa kijiji hicho kutokuwa
tayari kuchangia nguvyu zao kwa kuleta viashiria ili madarasa yaweze kujengwa
na kutengeneza madawati.
Wadau wa
elimu wakiwemo waandishi wa habari katika Wilaya ya Bunda, walisema kuwa hii ni
changamoto kubwa kwa shule hiyo, ambayo wakazi wake ni wafugaji na wakulima
ambao wamekuwa wakizalisha mazao mengi ya pamba na mtama, huku wakiwa na mamia
ya mifugo hususani ng’ombe, mbuzi na kondoo.
Walisema
kuwa iwapo wakazi wa kijiji hicho wakiwa tayari kujitoa na kuchangia nguvu zao,
ikiwa ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya hiyo, ambayo uchumi wake unatokana na
kilimo, madini, mifugo na uvuvi, shule za Wilaya hiyo kamwe haziwezi kukosa
vyumba vya madarasa, madawati, nyumba za walimu na nyingine kufungwa kwa kukosa
matundu ya vyoo.
Hivi
karibuni mwandishi wa habari hizi alishuhudia shule ya msingi Machimweru,
ambayo pia iko pembezoni, baadhi ya wanafunzi wakiwa wanasomea nje kwenye miti, huku idadi kubwa ya wanafunzi wake wakiwa wanasoma
wakiwa wamekaa kwenye mawe kwa kukosa madawati.
No comments:
Post a Comment