Na Ferdinand
Shayo, Arusha
Vijiji 120 vilivyopo mkoa wa Arusha vinatarajia kufikiwa na
huduma ya umeme kupitia mpango wa kusambaza umeme vijijini unaofadhiliwa na (REA)
na kutekelezwa na shirika la umeme la taifa (TANESCO).
Ofisa Uhusiano na Huduma kwa wateja ,TANESCO Arusha, Benedict Nkini amesema kuwa wako katika awamu ya pili ya
utekelezaji wa mradi huo wa umeme vijijini
na kwasasa wanaelekea katika wilaya za Arumeru, Karatu, Monduli na Longido
lengo ni kuhakikisha wananchi waishio vijijini wanafikiwa na huduma hiyo
muhimu.
Benedict Nkini akizungumza katika mkutano na Wananchi wa Vijiji vya Meserani juu na chini amesema kuwa kwa sasa wako katika hatua ya
kutoa elimu kwa wananchi juu ya mradi huo ili waweze kujiandaa kuunganishwa na
huduma hiyo na pia amewataka waepuke vishoka ambao hutumia uelewa mdogo wa wananchi
kujinufaisha.
Afisa Masoko wa Tanesco,Adelina Lyakurwa amesema kuwa
amewaomba wananchi kutumia fursa hiyo kuunganishiwa umeme huo wa bei nafuu
ambao Mtanzania wa hali ya chini anaweza kuumudu ,ambapo Mwanakijiji atatakiwa
kuwa na kiasi cha shilingi 32900 ili aweze kuunganishiwa umeme.
“Tunawaunganishia umeme watu wote wenye nyumba za
mawe,matofali,mbao kwa hiyo tunawaomba
wananchi watoe ushirikiano ili kufanikisha mradi huu,kwa upande wa nyumba za
nyasi na makuti kunahitajika ushauri wa kitaalamu kwasababu za kiutaalamu ili
kuepuka moto ambao unaweza kutokea kutokana na hitilifu ndogo” Alisema Afisa
Masoko.
Kaimu Mkurugenzi wa TANESCO wilaya ya Monduli0, Ramadhani
Mkayala amewataka wananchi watafute wakandarasi wazuri waliodhinishwa na
shirika ili kuepuka vihatarishi vya moto
Kwa upande wao wananchi wa Wilaya ya Monduli Sophia Mligo wa
kijiji cha Miserani na Gasper Lengta
wamesema kuwa wameupokea mpango huo
vizuri na kuwaomba TANESCO wazidi kufanya ushirikishaji zaidi na
wananchi ili uweze kufanikiwa bila vikwazo.
“Kuna wakati tulihisi kuwa serikali imetusahau watu wa
vijijini lakini sasa tunafarijika kuona hawa REA na TANESCO wanakuja
kutuunganishia umeme na tayari wameanza kuchimba mashimo kwenye kijiji chetu
shughuli iliyobaki ni kufukia nguzo ,uhakiki ulishafanyika hapo awali” Alisema
Parirong’o Sipitieki ambaye ni
Mwenyekiti wa Kijiji cha Ingoikumeni.
No comments:
Post a Comment