HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 19, 2014

SHIRIKA LA NYUMBA LATOA MASHINE 28 ZA KUFYATULIA MATOFALI KWA VIJANA MKOANI PWANI


 Meneja wa Shirika la Nyumba mkoa wa Pwani, Pauline Mrango akisoma Hotuba ya makabidhiano ya mashine 28 za kufyatulia matofali kwa vikundi vya vijana katika halmashauri zote za mkoa wa Pwani. Shirika la Nyumba la Taifa limetoa mashine hizo zenye gharama ya zaidi ya shilingi milioni 12 pamoja na mafunzo kwa vijana ya wiki mbili ambapo baada ya kumaliza mafunzo Shirika litatoa msaada wa shilingi laki tano kwa kila kikundi kama mtaji .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpa mkono wa pongezi Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa pwani Pauline Mrango kwa kutoa mashine 28 za kuwasaidia vijana.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria makabidhiano ya mashine za kufyatulia matofali zilizotolewa na shirika la nyumba la Taifa kwenda kwenye halmashauri zote za mkoa wa Pwani.
Mashine 28 zitawasaidia vijana mkoa wa Pwani kuondokana na tatizo la ajira, pili litasaidia sana katika utunzaji wa mazingira, zitasaidia wananchi kujenga nyumba za kisasa na kwa bei nafuu.

No comments:

Post a Comment

Pages