HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 17, 2014

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA KONGAMANO LA WATAFITI WA UFUGAJI NYUKI BARANI AFRIKA

 Mtendaji Mkuu wa wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Juma Mgoo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kongamano la sekta ya ufugaji nyuki Barani Afrika linalotarajiwa kufanyika Jijini Arusha kuanzia tarehe 11-16 Novemba, 2014. Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Ufugaji Nyuki Duniani Gilles Ratia, kulia ni Msemaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii Nurdin Chamuya. (Picha na Ismail Ngayonga- MAELEZO)
 Kaimu Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Gladness Mkamba (katikati) akizungumza na waandishi  wa habari kuhusu kongamano la sekta ya ufugaji nyuki Barani Afrika linalotarajiwa kufanyika Jijini Arusha kuanzia tarehe 11-16 Novemba, 2014. Kushoto ni Afisa Nyuki Mwanadamizi, Stephen Msemo, kulia ni Mtendaji Mkuu wa wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Juma Mgoo.
Mtendaji Mkuu wa wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Juma Mgoo (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kongamano la sekta ya ufugaji nyuki Barani Afrika linalotarajiwa kufanyika Jijini Arusha kuanzia tarehe 11-16 Novemba, 2014. Kushoto Kaimu Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Gladness Mkamba.

Na Ismail Ngayonga, MAELEZO, Da es Salaam

TANZANIA inatarajia kuwa mwenyeji wa kongamano la  watafiti na wanasayansi wa sekta ya ufugaji nyuki Barani Afrika linalotarajiwa  kufanyika Jijini Arusha kuanzia tarehe 11 hadi 16 Novemba mwaka huu.

Kongamano hilo linatajiwa kuhudhuriwa na washiriki 550 ambapo kati yao Watanzaniani 250 na wageni kutoka nje ya nchi wanatarajia kuwa 300.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo Jumanne (Septemba 16, 2014), Jijini Dar esSaalaam, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Misitu Tanzania katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Juma Mgoo alisema lengo la kongamano hilo ni kuimarisha sekta ndogo ya ufugaji nyuki kwa kushirikisha wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Aliongeza kuwa katika kongamano hilo wadau hao pia watajadili kwa pamoja namna bora zaidi ya kusaidia mchango wa sekta hiyo katika Nyanja zautafiti, teknolojia pamoja na kubadilishana uzoefu katika uboreshaji, utunzaji na usimamizi wa makundi ya nyuki kwa uzalishaji wenye wingi na ubora.

“Kongamano litahusisha uwasilishwaji wa mada za utafiti kwa njia za mijadala, semina kwa wafugaji nyuki, majadiliano ya kitaalamu sanjari na maonyesho ya bidhaa za ufugaji nyuki” alisemaMgoo.

Aidha Mgoo alisema washiriki wote watapaswa kujilipia ada ya ushiriki ikiwemo gharama za usafiri na malazi, ambapo kwa kutambua ukubwa wa gharamahizo Serikali ililazimika kulipia baadhi ya huduma.  “Gharama za mtu mmoja kwa siku ni dola za kimarekani 120 ila mshiriki wa Tanzania hulipaTsh. 150,000/- tu” alisema Mgoo.

Kwa mujibu wa Mgoo mbali na kongamano hilo, washiriki hao pia watapata fursa ya kushiriki ziara ya mafunzo, kwa kutembelea  maeneo mbalimbali yanayojihusisha na ufugaji nyuki nchini ikiwemo Mkoawa Kilimanjaro, ambapo wataweza kujionea ufugaji nyuki wasiouma pamoja na ufugaji nyuki katika nyanda kame za Mikoa ya Singida na Dodoma.

Kwa wake upande Rais wa Shirikisho la UfugajiNyuki Duniani (Apimondia) Gilles Ratia amesifu maandalizi mbalimbali yanayofanywa na Serikali ya Tanzania katika kufanikisha na kuwezesha mkutano huo nchini.

Akizungumzia sekta ya ufugaji nyuki nchini, Ratia amepongeza jitihada kubwa zilizofanywa na Serikali katika kuwasaidia na kuwaendeleza wafugaji wa nyuki, na hivyo kuwataka wafugaji kujitokeza kwa wingi kushiriki  kongamano hilo litakaloweza kuwajengea uwezo katika uzalishaji na hivyo kuwaongozea kipato.
“Napenda kutoa pongezi zangu kwaMhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwaj itihada zake anazozionyesha katika kusaidia na  kuendeleza sekta ya ufugaji nyuki kwani ameonyesha nia ya dhati ya kusaidia sekta hii” alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages