HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 31, 2014

KUKATIKA KWA UMWEME DAR TANESCO WAOMBA RADHI

Na Mwandishi Wetu
 
SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO), imesema tatizo la kukosekana kwa huduma hiyo katika baadhi ya maeneo kulikojitokeza wiki iliyopita kulisababishwa usafishaji wa visima vya gesi ya Songosongo.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Flechesmi Mramba, alisema Kazi hiyo ilikuwa ikifanywa na Kampuni Pan African ambayo ndio inayosimamia visima hivyo.

Alisema, kazi hiyo ilisababisha ratiba ya uaptikanaji wa gesi kubadilika hali iliyofanya wakati mwingine wajikute hali yakukosa huduma hiyo.

Mramba, alisema kutokana na ratiba hiyo walilazimika kutumia mitambo ya mafuta ili kuziba upungufu huo kutokana na mahitaji makubwa.

Hata hivyo kutokana na mahitaji hayo makubwa wakati mwingine Tanesco imejikuta ikikosa mafuta hali iliyosababisha usumbufu kwa wateja.

"Tunawasilana na watu wa Songosongo wametuhakikishia kuwakazi ya usafishaji visima hivyo inakwenda vizuri inaitamalizika, kufanaya tatizohilo kumalizika kesho na kwamba tuwaombe radhi wateja na pia wajue sababu iliyosabisha usumbufu huu,"alisema Mramba.

Aidha, alisema hivi sasa katika kumaliza matatizo ya umeme katika baadhi ya maeneo Mbagala Tanesco imeamua kujenga laine nyingine kutoka Kipawa kwenda Mbagala ambayo itasaidia laini inayotoka Ilala iliyozidiwa na wateja.

Baada ya kukamilika line hiyo anamini kuwa hali ya upatikanaji wa huduma hiyo katika maeneo ya Mbagala na mengine itakuwa nzuri.

No comments:

Post a Comment

Pages