HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 23, 2014

NSSF YAENDESHA SEMINA KWA WAAJIRI, WANACHAMA

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hab Mkwizu (katikati), Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori (kulia) na Meneja Idara za Serikali na Balozi NSSF, Rehema Chuma wakiwasili kwenye ukumbi wa mikutano wakati wa semina ya wadau wa Kada ya Utumishi wa Idara na Asasi za Serikali iliyoandaliwa na NSSF mjini Bagamoyo.


Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori  akitoa akifafanua jambo wakati wa semina ya wadau wa Kada ya Utumishi wa Idara na Asasi za Serikali iliyoandaliwa na NSSF na kufanyika mjini Bagamoyo, mwishoni mwa wiki. Wa pili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hab Mkwizu, Meneja wa Idara za Serikali na Balozi NSSF, Rehema Chuma  na Meneja wa NSSF Mkoa wa Kibaha, Ummy Lweno. 
 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hab Mkwizu akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa semina ya wadau wa Kada ya Utumishi wa Idara na Asasi za Serikali iliyoandaliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na kufanyika mjini Bagamoyo.
 Meneja wa Idara za Serikali na Balozi NSSF, Rehema Chuma akizungumza katika semina hiyo.
  Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori  akitoa mada wakati wa semina ya wadau wa Kada ya Utumishi wa Idara na Asasi za Serikali iliyoandaliwa na NSSF na kufanyika mjini Bagamoyo.
 Baadhi ya washiriki wa semina hiyo.
 Washiriki wa semina wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwakilishwa.
 Wadau wa NSSF wakiwa katika mkutano huo.
 Maofisa wa NSSF wakiwa katika mkutano huo.
 Maofisa wa NSSF wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa.
Meneja wa Idara za Serikali na Balozi NSSF, Rehema Chuma (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala, Chiku Matesa.
 Mgeni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hab Mkwizu (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa semina hiyo.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hab Mkwizu akiagana na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori mara baada ya kufungua semina ya wadau wa Kada ya Utumishi wa Idara na Asasi za Serikali iliyoandaliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na kufanyika mjini Bagamoyo jana. Katikati ni Meneja Idara za Serikali na Balozi NSSF, Rehema Chuma.
  
Na Mwandishi Wetu

NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hab Mkwizu, amewataka waajiri na wanachama wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kujadili changamoto zinazokabili shirika hilo na kuzitatua.

Mkwizu aliyasema hayo mjini Bagamoyo katika semina iliyoandaliwa na NSSF ikiwa ni utaratibu wa shirika hilo kukutana na wadau wake.

Alisema kuwa dhana nzima ya hifadhi ya jamii bado haieleweki kwa wafanyakazi wengi na hiyo ni moja ya changamoto inayokabili mifuko hiyo ndani ya nchi.

Mkwizu alisema changamoto nyingine ni wanachama kustaafu bila kujua ni mfuko upi wanapaswa kwenda kufungua madai yao pensheni.

Aliwataka NSSF kutumia semina hiyo kutoa elimu na uelewa juu ya dhana nzima ya hifadhi ya jamii, shughuli za shirika na mafao yanayotolewa kwa wanachama, tararibu za kujiunga na taratibu za kufungua madai baada ya mfanyakazi kustaafu.

Meneja wa Idara za Serikali na balozi NSSF, Rehema Chuma, alisema semina hiyo ni uendelezaji wa elimu kwa wananchi na waajiri, kujenga mahusiano ili kushughulikia maslahi ya wafanyakazi, kuelewa na kujadili changamoto mbalimbali za sekta hii.

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Crescentius Magori, alisema  changamoto zitakazopatikana zitasuluhishwa na kuongeza kuwa NSSF ni mfuko unaotoa mafao ambayo mifuko mingine haina likiwemo fao la uzazi na matibabu.

No comments:

Post a Comment

Pages