utumishi katika kanisa hilo.
Hayo yalisemwa na Askofu wa kanisa hilo Mahimbo Mndolwa wakati alipokuwa akizungumza kuhusu sherehe ya kumuaga mchungaji wa kigango cha Mashewa Thomas Ngereza, iliofanyika katika Kanisa ST. Andrews Manundu wilayani Korogwe Mwishoni mwa wiki.
Askofu Mndolwa, alisema kuanzishwa kwa mafao hayo ya uzeeni kutasaidia mhusika wakati atakapostaafu aepukane na maisha magumu yatakayowafanya wageuke kuwa ombaomba.
“Leo kwa pamoja tukiongozwa na Mwenyekiti wetu Dominic
Singano tumemzawadia mstaafu mabati 59,
mbao, misumali kilo 10 pia alikabidhiwa cheti,”alisema Mndolwa.
Askofu Mndolwa, aliyataja baadhi ya mafao ambayo atayopatiwa mstaafu ni kama
vile nyumba, gari na fedha, ambayo anaamini kuwa yatamsaidia mstaafu huyo katika
kupambana na changamoto mbalimbali za maisha.
Licha ya kumuaga mchungaji Ngereza pia walikuwepo watumishi wengine
wanne waliostaafu kutoka katika Taasisi ya Afya na
Sayansi Shirikishi ya St. Agustino ya wilayani
Muheza ambao ni Mery Dismasi,Charles Juma, Peter Rajabu na Itikija Mbaga.
Askofu mstaafu wa Aglicana Dayosisi ya
Tanga Philip Baji, alikemea tabia za baadhi ya wachungaji ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya wizi wa
sadaka.
Askofu mstaafu wa Aglicana Dayosisi ya
Tanga Philip Baji, alikemea tabia za baadhi ya wachungaji ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya wizi wa
sadaka.
Sherehe hiyo ilihudhuriwa na Askofu mkuu mstaafu Anglicana Verentino Mokiwa kutoka jijini Dar, Askofu wa Anglikana Dayosisi ya Zanzibar Michael Afizi na Padri Joseph Mhina.
No comments:
Post a Comment