Mwanamke wa India katika kile kinachoonekana kuwa maajabu
ya dunia ya aina yake kuwahi kutokea duniani amefanikiwa kujifungua
salama watoto wafuatao 11 (kumi na moja) kwa mara moja, jambo ambalo
wauguzi na madaktari wote bingwa hawajawahi kuliona popote pale
Hospitalini walipowahi kutoa huduma kwa wajawazito,bali hata kwa
hospitali zote za dunia hakujawahi kusikika kitu cha namna hiyo.
Picha ya mama huyu akiwa na watoto wake 11 imeutikisa
mtandao wa Internet na kufanikiwa kujichukulia headline katika magazeti
mbali mbali ya dunia ya kila siku, ikiwa na anuani ifuatayo:
"Mwanamke wa Kihindi ajifungua Timu ya Taifa yenye jumla ya wachezaji 11".
Vyanzo vya Habari vya India vimesema kwamba:Mama huyo
aliyetajwa anatoka katika familia ya kimaskini na amejaribu kuelekea
katika moja ya Hospitali za umma za Serikali ya India ili kujifungua,na
mumewe ni mfanyakazi katika moja ya maduka ya Ubani (au Uvumba).
Vyanzo vimeongeza kuwa:Timu ya madaktari imeshangaa sana,
na kilichowashangaza zaidi ni ule ukubwa wa tumbo la mama mjamzito ambao
hauendani sawa na urefu wake pamoja na ukubwa wa mwili wake,na kwamba
kuzaliwa watoto idadi hii kumewaacha midomo wazi
wasimamizi,wauguzi,madaktari, na utawala mzima wa hospitali,bali
hata kila aliyekuwepo katika Hospitali hiyo wakiwemo wagonjwa na wale
walio zimia na kupoteza fahamu,nao wameshangaa.
Hospitali hiyo ghafla imejikuta ikigeuka kuwa sehemu ya kivutio kwa wale walio miminika mahala hapo ili kushangaa shangaa na kutizama watoto hao mapacha 11 waliotimia maguu duniani.
No comments:
Post a Comment