HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 22, 2015

MAENDELEO BANK YAZINDUA HUDUMA MPYA YA MB MOBILE

Naibu wa Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya MB Mobile ya Maendeleo Benki uliofanyika jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)
Naibu wa Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba (wa tatu kushoto) akizindua huduma mpya ya MB Mobile ya Maendeleo Benki uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Banki, Ibrahim Mwangalaba, Mkurugenzi wa Benki hiyo, Balozi, Richard Mariki na Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dk. Alex Malasusu.
Tunazindua...............???
Tumezindua.......huduma mpya.
Huduma mpya ya MB Mobile yazinduliwa.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa mara baada ya kuzindua huduma mpya ya MB Mobile 
Mmeona zawadi niliyopewa...................????
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba (katikati) akiteta jambo na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa mara baada ya kuzindua huduma mpya ya MB Mobile.
Picha ya pamoja ya wakaurugenzi.
Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa Maendeleo Bank
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba (katikati) akibadilishana mawaz na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa (kulia) mara baada ya kuzindua huduma mpya ya MB Mobile

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania kujenga utamaduni wa kuweka akiba kwa ajili ya maendeleo endelevu.

Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam katika uzinduzi wa  huduma mpya ya 'MB mobile' ulioanzishwa na Benki ya Maendeleo.
Alisema ili Nchi yoyote duniani ipige hatua uwekaji wa akiba ni jambo muhimu sana, hivyo Watanzania wanapaswa kujenga utamaduni huo ili kwani ndio njia pekee ya kujipatia maendeleo kwa urahisi.

Mwigulu alisema hiyo ni hatua mojawapo ya maendeleo ambayo benki hiyo imepiga kwani hivi sasa wateja wao hawatapata shida ya kuhangaika kuweka au kutoa fedha.

"Benki ya Mkombozi haina muda mrefu lakini inaonekana inapiga hatua kubwa kimaendeleo, hivyo nawaomba Watanzania wasiwe na hofu kuweka akiba katika benki hii kwani fedha zao zitakuwa sehemu salama," alisema Nchemba.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Ibrahim Mwangalaba, alisema benki yao ina mwaka mmoja na miezi mitatu tangu ianzishwe lakini wanashukuru wanakwenda vizuri.

Alisema hadi sasa ina wateja 7,000 na wameweza kukusanya amana zaidi ya sh. bilioni 15.5 na pia imechangia kuongeza kasi ya ukuaji uchumi nchini kwa kutoa mikopo ya zaidi ya sh. bilioni 10.

Aliongeza kuwa kupitia huduma hiyo mpya ya MB Mobile wateja wataweza kutumia huduma ya kifedha bila kujali eneo, kwa kuangalia salio, kuweka pesa kwenye akaunti zao kwa kupitia Tigo pesa na M-Pesa.

No comments:

Post a Comment

Pages