HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 27, 2015

Miaka 15 ya Tamasha la Pasaka

Lilivyokuwa Tamasha la Pasaka mwaka 2000

Na Mwandishi Wetu

WAKATI tukielekea kwenye Tamasha la Pasaka ambalo linatarajia kufikisha miaka 15 tangu kuasisiwa kwake, tujikumbushe baadhi ya matukio ambayo yaliyotokea katika matamasha yaliyopita.

Kwa kuwa lilikuwa ni tamasha la mwanzo ambalo liliandaliwa na Kampuni ya Msama Promotions yenye maskani yake Kinondoni jijini Dar es Salaam, kulikuwa na changamoto nyingi kwa sababu ya ugeni katika uandaaji wa matamasha.

Mojawapo ya changamoto zilizojitokeza katika tamasha la kwanza  ni kuzuiwa na wamiliki wa ukumbi wa Diamond kwa deni la shilingi 300,000 ambazo zililipwa baadaye.

Kadri miaka inavyokwenda mbele, Kampuni ya Msama inapiga hatua taratibu kwa sababu ya ufanisi wa Kamati ya Maandalizi.
Katika tamasha hilo la kwanza mgeni rasmi alikuwa rais wa awamu ya pili, Ali Hassani Mwinyi , hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya waimbaji waliopanda jukwaani mwaka huo ni Marehemu Angela  Chibalonza, Kwaya ya Lulu Mtoni, Jangala Son, Mzungu Four na Faustine Munishi  ambaye anaendelea na shughuli zake nchini Kenya.

Itaendelea wiki ijayo…..

No comments:

Post a Comment

Pages