HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 06, 2015

KAMISHINA WA TRA ATINGA BARAZA LA MAADILI KUHUSU MGAO WA FEDHA ZA ESCROW

 Naibu Kamishna Upelelezi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Loicy Appolio, akiwa mbele ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma jana, ambapo anatuhumiwa kupokea mgawo wa shs. milioni 80.85 kutoka kwa mmiliki wa Kampuni ya VIP Engineering and Marketing Limited, James Rugemalira. (Picha na Francis Dande)


Na Mwandishi Wetu

NAIBU Kamishna Upelelezi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Loicy Appolio, leo amefuata nyao za watangulizi wake watatu kupinga kuhojiwa na Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma na baadala yake amekimbilia Mahakama Kuu kuweka pingamizi.

Watangulizi hao watatu waliokimbilia Maahakamani kupinga kuhojiwa kuhusu tuhuma za kupokea mgao wa fedha toka Kampuni ya VIP Engineering and Marketing Limited, ni Mwanasheria Mkuu wa zamani Endrew Change, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Wizara ya Nyumba ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rogonzibwa Mujunangoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajaili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Philip Saliboko.

Loicy, anatuhumiwa kupokea mgawo wa sh.milioni 80.85 kutoka kwa mmiliki wa kampuni hiyo, James Rugemalira, ni kinyume cha sheria ya maadili ya viongozi wa umma.

Pia analalamikiwa kuwa hakutamka kwa kamishna wa maadili, Hotel anayoimiliki inayoitwa ‘Clasic Hotel yenye thamani ya sh. milioni 150 iliyoko Kinondoni ambayo katika tamko lake la rasilimali na madeni kwa kipindi kilichoishia Desemba 31, mwaka (2010, 2011, 2012, 2013 na mwaka 2014).

Wakili Ogunde aliwasilisha pingamizi hilo baada ya Wakili wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Filotheus Manula kuwasilisha malalamiko hayo dhidi ya Loicy mbele ya baraza hilo.

Wakili Ogunde aliwasilisha pingamizi hilo baada ya Loicy kukana malalamiko yote yaliyowasilishwa na Wakili Manula dhidi yake.

 Akiwasilisha pingamizi hilo, Wakili Ogunde alidai baraza halina uwezo wa kusikiliza malalamiko dhidi ya mteja wake kwa madai kwamba  kuna amri ya zuio iliyotolewa na Mahakama Kuu kwa chombo chochote cha umma kushughulikia suala lolote linalohusu kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) pamoja linalohusu akaunti ya Tegeta Escrow.

 Alidai zuio hilo lilitolewa kupitia kesi ya msingi namba 5 ya mwaka 2014 iliyofunguliwa na IPTL na wenzake dhidi ya Waziri Mkuu na wenzake saba na kwamba, baraza lina nakala ya amri hiyo.

Hatua iliyochukiliwa na Loicy ni sawa na ile iliyochukuwa na mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na wenzake wawili, alipofikishwa mbele ya baraza hilo hivi karibuni.

Hata hivyo, Jaji Msumi, alimweleza wakili Ogunde kuwa katika shauri dhidi ya Chenge, waliona baraza lina uwezo wa kusikiliza kwa sababu baraza si sehemu ya waliopewa amri hiyo ya zuio na Mahakama Kuu.

Kauli ya Jaji Msumi ilijibiwa na Wakili Jamhuri, ambaye alidai amri ya zuio hilo inavihusu vyombo vya umma na kwamba, baraza ni chombo cha umma, ambavyo vimezuiwa kuendelea kushughulikia suala hilo hadi kesi hiyo ya msingi iliyopo Mahakama Kuu itakaposikilizwa na kuamuliwa.

Hoja hizo za Wakili Ogunde zilipingwa na Wakili Manula huku akiomba muongozo kutoka kwa Jaji Msumi kwamba mapingamizi  hayo yatachukuwa muda gani hivyo kuomba kesi hiyo iendelee.

Kabla ya Jaji Msumi kujibu muongozo huo alimueleza Wakili wa serikali kuwa suala lililokuwa mbele yao lilkuwa tofauti na yale yaliyotangulia kwani hili likuwa nalinahusu kesi mbili tofauti.

“Niombe kuwa wakati mwingine mkajipanga katika fuata sheria kwa kuorodheshamashauri haya kwa namba ambazo zitafafanua adhabu kwa kila makosa,”alieleza Jaji Msumi.

Jaji Msumi alieleza hivyo baada ya kubaini katika tuhuma zilizowasilishwa  kulikuwa na suala lingine linalohusu Hoteli inayoitwa ‘Classic Hotel’ ambayo inathamani ya sh. milioni 150, ambalo nalo hili ni suala kubwa mno.


Akijibu muongozo uliyombwa na wakili wa serikali kuhusu kikomo cha mapingamizi kwamba yatachukua muda gani, elieleza kuwa itategemea wahusika kuharakisha mchakato wa kuwakirisha rifaa zao katika Mahakama Kuu pia waelewe kuwa kuna muda wa kufanya hivyo na wasijidanganye kama wanaweza kuchelewesha muda.

No comments:

Post a Comment

Pages