HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 01, 2015

BENKI YA CRDB YAVUTIA WENGI MAONYESHO YA SABASABA

Dar es Salaam, Tanzania 

BENKI ya CRDB imewataka Watanzania kutembelea banda lao ili kupata huduma mbalimbali za Fedha.

Akizungumza katika Maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama sabasaba yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba, Ofisa wa benki hiyo, John Titus amesema kuwa banda lao linashughulika na kufungua akaunti na kumuhudumia mteja.

Aliongeza kuwa Benki ya CRDB pia imeweka Mobile  Branch ambayo hufanya kazi zote zinazofanywa na benki hiyo ikiwemo huduma za kuweka fedha na kutoa.

Titus alisema pia wanahuduma ya Jumbo ambayo ni akaunti kwa ajili ya watoto.

Alisema akaunti hiyo huwapa watoto fursa ya kuwekezewa fedha zitakazowasaidia katika masomo na maisha yao ya baadae.

Wateja wa Benki ya CRDB wakipata huduma za Fedha katika Mobile Branch katika maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba Barabara ya Kilwa.
Wateja wa Benki ya CRDB wakipata huduma za Fedha katika Mobile Branch katika maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba Barabara ya Kilwa.
Gari aina ya Passo ambayo itakabidhiwa kwa mshindi wa mwezi Juni katika viwanja vya Sabasaba.
Ofisa wa Benki ya CRDB, David John akitoa ufafanuzi kuhusu Huduma ya Simbanking kwa mteja aliyefika katika banda la CRDB katika maonyesho ya Sabasaba.
Ofisa Mauzo wa Benki ya CRDB, Iyvonne Millinga akimuhudumia mteja kwenye maonyesho ya Sabasaba.
Mteja akiweka sahihi baada ya kufungua akaunti. 
Ofisa Mauzo wa Benki ya CRDB, Pamela Haule akitoa huduma kwa Hawa Hashimu ambaye aliyefika kufungua akaunti katika Viwanja vya Sabasaba.
Ofisa Mauzo wa Benki ya CRDB, Pamela Haule akitoa huduma kwa wateja waliofika katika banda la benki ya CRDB.
Ofisa wa Benki ya CRDB, John Titus (katikati) akimuhudumia mteja wa benki hiyo aliyefika katika banda la benki hiyo, Gerald Stanslaus katika maonyesho ya Sabasaba.
Wateja wakipata huduma katiba banda la CRDB.
Mteja akiweka Passworld baada ya kufungua akaunti. 
Wateja wakipa huduma katika Mobile Branch.

No comments:

Post a Comment

Pages