Mgombea ubunge jimbo la Itilima (Bariadi Mashariki), Njalu Silanga (CCM), akiwasili katika kijiji Zanzui Mlimani wakati wa mkutano wa kampeni. (Picha na Loveness Bernard)
Na Mwandishi wetu, Bariadi
Na Mwandishi wetu, Bariadi
Mgombea ubunge jimbo la itilima (Bariadi mashariki)Njalu
Silanga kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) amewaomba wananchi
kuchagua Chama hicho ili waweze kupata suluhisho la matatizo yao.
Njalu amesema hayo katika mikutano ya kampeni za kuomba
kuchaguliwa kuwa mbunge katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika
mwezi huu nchini kote alipokuwa kata za Ndoleleji na Migato.
''Tunaomba mchague CCM kwani ndio Chama bora ambacho
kinaweza kutatua shida zenu kwani wanazijua na wanaweza kuwatatulia
kwani ilani yao ya uchaguzi imeelezea namna yakukabiliana na kutatua
matatizo.
Aidha amewataka wananchi kutokujihusisha na vurugu zozote
ambazo watashinikizwa na watu mbalimbali kwani wanaweza kuumia, kufungwa
ama kuachwa na vilema vya maisha
Mgombea ubunge jimbo la Itilima (Bariadi Mashariki), Njalu Silanga (CCM), akimsalimia mtoto mdogo katika kijiji Zanzui Mlimani.
Mgombea ubunge CCM jimbo la Itilima (Bariadi Mashariki), Njalu Silanga akimsalimia mtoto mdogo katika kijiji Zanzui Mlimani.
No comments:
Post a Comment