Msemaji
wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud, akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu kupatikana kwa watu 5
walioangukiwa na kifusi kwa siku 41 katika
machimbo ya Nyangalata Kahama mkoani Shinyanga. Kulia ni Ofisa habari Idara ya
Habari (Maelezo), Jackiline Mrisho. (Picha na Loveness Bernard)
Na
Jacquiline Mrisho- Maelezo
Wachimbaji
wadogo wadogo waliofukiwa katika mgodi
wa Nyangalata ulioko wilayani Kahama wamepatikana wakiwa hai.
Hayo
yamesemwa na msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Bi. Badra Masoud alipokua
akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuwa wachimbaji hao
walikaa kwa muda wa siku 41 kuanzia tarehe 5, oktoba hadi tarehe 15, novemba
2015.
Msemaji
huyo amewataja wachimbaji hao waliookolewa wakiwa hai ni Muhangwa Amosi, Joseph
Bulule, Chacha Wambura, Msafiri Gerald na Onyiwa Aindo ambao mpaka sasa wako
katika Hospital ya wilaya ya Kahama wakiendelea na matibabu kwakua hali zao
hazikuwa nzuri.
Aliongeza
kuwa mmoja kati ya wachimbaji hao Bw. Musa Supana alifariki dunia siku 15
zilizopita na mwili wake bado haujaonekana hivyo uongozi wa Wilaya kwa
kushirikiana na wachimbaji wadogowadogo wanaendelea kuutafuta mwili huo.
Aidha,
Bi. Badra aliongeza kuwa wachimbaji hao waliishi maisha ya shida kwa kula
magome ya miti na kugawana maji kidogo yaliyokua yakidondoka.
Hata
hivyo Wizara inatoa ruzuku na mikopo ili uchimbaji uwe wa kisasa na kutoa wito
kwa wachimbaji wachimbe kwa kutumia nyenzo za kisasa na kuwa makini katika shughuli za uchimbaji.
No comments:
Post a Comment