HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 18, 2016

AIRTEL YAZINDUA KAMPENI YA MR. MONEY KUPITIA HUDUMA YA AIRTEL MONEY

  • Mr. money amezinduliwa kuleta urahisi na Uhakika kwa watumiaji wa Airtel Money
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imetambulisha na kuzindua kampeni yake mpya kwa wateja kupitia huduma yake yake yakifedha kwa njia ya Mtandao ya Airtel Money  
Kampeni hiyo imezinduliwa katika ukumbi wa burudani/club wa Maisha basement jana usiku mbele ya waandishi wa habari na watangazaji wa vipindi vya redio toka redio mbalimbali huku Meneja wa huduma ya Airtel Money  Moses Alphonce akitoa sababu za ujio wa Mr. Money  kwamba amekuja na habari za unafuu urahisi na usalama unaopatikana kupitia huduma ya Airtel Money sasa ambapo huwezi kupata kwingine.
Akiongea wakati wa uzinduzi wa  Mr Money Meneja huyo alisema "Mr. Money anasema ‘tumia Airtel Money kwa kuwa ndio nafuu na hakika kuliko mitandao yote’ Kutuma pesa popote nchini ni BURE na kwa uhakika Lipia BILI kama LUKU na ujipatie nyongeza za unit za umeme, hii ni kwa Airtel money TU
Au lipia Ving’amuzi kwa uhakika  na kwa raha bila usumbufu
Pia Ongeza salio popote ulipo kwa uhakika, utapata bonasi ya muda wa maongezi BURE
Ukiwa na airtel money unaweza kufanya mengi Zaidi.
Meneja wa Msoko wa Airtel Money, Moses James (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wakati wa hafla ya kutambulisha huduma mpya ya Mr. Money, itakayomwezesha mtumiaji wa Airtel Money kurahisisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu ya mkononi. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando na Meneja wa Airtel Money, Asupya Nalingigwa.
Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi usiku, wakati wa hafla ya kutambulisha huduma mpya ya Mr. Money, itakayomwezesha mtumiaji wa Airtel Money kurahisisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu ya mkononi. Kulia ni na Meneja wa Airtel Money, Asupya Nalingigwa na Meneja wa Msoko wa Airtel Money, Moses James.
 Sehemu ya wafanyakazi wa Airtel Tanzania wakifuatilia jambo, wakati wa hafla ya kutambulisha huduma mpya ya Mr. Money, itakayomwezesha mtumiaji wa Airtel Money kurahisisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu ya mkononi, iliyofanyika  jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages