Balozi wa Kili Challenge ambaye pia ni msanii wa muziki wa kughani, Mrisho Mpoto akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu tukio la kupandisha watu 50 katika kilele cha mlima Kilimanjaro na waendesha baiskeli 50 watakaozunguka mlima huo kwa baiskeli ili kuchangisha fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi. Kulia ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), Tenga Tenga. na kushoto ni Kamishina wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Peter Dickson.
Balozi wa Kili Challenge ambaye pia ni msanii wa muziki wa
kughani, Mrisho Mpoto akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam, kuhusu tukio la kupandisha watu 50 katika kilele cha
mlima Kilimanjaro na waendesha baiskeli 50 kuuzunguka mlima huo kwa baiskeli
ili kuchangisha fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi. Kulia ni Meneja
Uhusiano na Mawasiliano wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), Tenga Tenga. (Picha
na Francis Dande)
NA FRANCIS DANDE
MGODI wa Dhahabu wa Mkoani Geita
ambao umekuwa ukishirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi tangu kuanzishwa kwake miaka
15 iliyopita, unataraji kupandisha watu 50 katika kilele cha mlima Kilimanjaro maarufu
kama ‘Kili Challenge’ ili kuchangisha fedha za
mapambano dhidi ya Ukimwi.
Mbali ya idadi hiyo kupanda
kileleni mwa mlima huo mrefu zaidi barani Afrika, kutakuwa na waendesha
baiskeli 50 ambao watazunguka mlima huo kwa baiskeli, yote hiyo katika kampeni
hiyo ya kusaka fedha
za kusaidia mapambano ya
ugonjwa wa Ukimwi.
Meneja wa Mawasiliano na
Mahusiano wa Mgodi wa GGM, Tenga Tenga, alisema
jana kwamba, tukio hilo limalovuta hisia za wengi kutoka ndani na nje ya
Tanzania wakiwamo wanaharakati wa vita dhidi ya ukimwi, litafanyika kuanzia
Julai 16 hadi Agosti 22.
“Kilimanjaro Challenge kwa
mwaka huu itakuwa na kundi kubwa la watu kutoka ndani na nje ya Tanzania , japo
wengi wao watakuwa kutoka hapa nchini wakiwamo kutoka sekta binafsi, serikalini,
wawakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN) waliojitolea kuchangia mfuko huo wa Kili
Challenge. Balozi wetu Mpoto ndiye ataambatana na kundi hili hadi kileleni,”
alisema Tenga.
Akizungumza jijini Dar es
Salaam leo, Mpoto amewasihi watanzania kutambua mapambano dhidi ya Ukimwi ni
jukumu la wote, hivyo ni jukumu la wote ili kufikia dhamira ya sifuri tatu kwa
maana ya kumaliza kabisa maambukizi mapya, unyanyapaa pamoja na vifo.
“Mimi kama
Balozi wa Kili Challenge naamini
jitihada zinazofanywa na mfuko huu
zinahitaji kuungwa mkono na watanzania wote na wadau wenye machungu na nchi
hii. Hebu tuungane kwa pamoja, kila
mmoja kwa sehemu yake, iwe kwa kuchangia ama kuelimisha mwingine ili mapmbano
haya yalete manadiliko,” alisema Mpoto.
Naye Mwakilishi wa Tacaids,
Dickson Peter, alisema fedha zitakazopatikana zitapelekwa kusaidia mapambano
dhidi ya ukimwi ikiwemo kujenga vituo
vya ushauri nasaha na upimaji wa ukimwi ambapo baadhi yao ni vile vilivyopo Segera Mkoani Tanga,
Manyoni na Geita.
Peter aliyataja matunda
mengine ya Kili Challenge, ni kituo cha watoto Yatima Moyo wa Huruma na asasi
nyingine zaidi ya 30 ambazo tayari zimenufaika na mfuko huu tangu uanzishwe na
kusema GGM, inatambua pia sapoti ya wadau
wengine kama Acacia, Prime Fuel, Artel, Capital
Drilling (T) Ltd na wengineo.
No comments:
Post a Comment