HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 28, 2016

YANGA YALALA 1-0 MBELE YA TP MAZEMBE

 Mashabiki wa Kongo wakiingia Uwanjani kushuhudia pambano la Kombe la Shirikisho Barani Afrika kati ya Yanga na TP Mazembe kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, katika mchezo huo TP Mazembe waliibuka kidedea baada ya kuifunga Yanga 1-0. (Picha na Francis Dande)
 Mashabiki wa Yanga kabla mpira kuanza.
Mashabiki wa Simba wamefurika katika jukwaa lao.
 Mashabki wakiingia Uwanjani.
 Mashabiki wakiwa nje ya uwanja.
 Mashabiki wakiwa wakiwa nje ya Uwanja wa Taifa baada ya uwanja kufurika mashabiki na kushindwa kuingia.
 Vijana wakikimbia baada ya Polisi kupiga bomu la machozi.
 Watu mbalimbali wakikimbia baada ya Polisi kuwatawanya kwa kupiga mabomu ya machozi.
 Mashabiki wa Soka wakikimbia mabomu ya machozi baada ya kutawanywa na Jeshi la Polisi.
 Watu mbalimbaliwakikimbia ovyo baada ya Polisi kuwatawanya mashabiki waliohudhulia pambano la Yanga na TP Mazembe.
 Tukimbie mabomu ya machozi.
 Polisi akipiga bomu la machozi.
 Askari Polisi akijiandaa kupiga bomu la machozi.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Siro akizungumza na vijana waliokusanyika nje ya Uwanja wa Taifa. 
 Kocha wa Yanga, Hans Pluijm (kulia), akizungumza na kocha wa TP Mazembe.
 Timu zikiingia uwanjani.
 Wachezaji wakisalimiana kabla ya mchezo.
 Benchi la ufundi la TP Mazembe.
 Golikipa wa TP Mazembe akiwapanga wachezaji wake.
 Beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Canavaro' akiwa na mshambuliaji wa TP Mazembe, Thomas Ulimwengu.
 Beki wa TP Mazembe, Christian Luyindama akiokoa hatari langoni mwake mbele ya mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma. 
  Beki wa Yanga, Juma Abdul akiwania mpira na kiungo wa TP Mazembe Roger Claverkatikamchezo wa Kombe la Shirikisho.
 Beki wa Yanga, Juma Abdul akimiliki mpira mbele ya mbele ya kiungo wa TP Mazembe Roger Claver katikamchezo wa Kombe la Shirikisho. 
 Niyonzima akiwania mpira.
 Kiungo wa TP Mazembe Roger Claver akichuana na Deus Kaseke katika mchezo wa Kombe la Shirikisho. 
Juma Mahadhi akimtoka Adama Traore.

No comments:

Post a Comment

Pages