Msafara wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya vijana wenye umri wa
chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, uliondoka jana alfajiri Dar es
Salaam, Tanzania imetua salama jijini Antananarivo, Madagascar kwa ajili
kambi ya siku 10 kujiandaa na mchezo dhidi ya Afrika Kusini kuwania
nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika utakaofanyika
Agosti 6, 2016.
Mchezo wa marudiano utafanyika Agosti 21, mwaka huu kwenye Uwanja wa
Azam, ulioko Chamazi-Mbagala, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam na
kwamba mshindi atakuwa amejiwekea mazingira mazuri ya kuwania nafasi ya
kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana, zitakazofanyika
mwakani huko Madagascar.
Mkuu wa msafara akiwa ni Ayoub Shaibu Nyenzi ambaye ni Mwenyekiti wa
Kamati ya Soka la Vijana, maofisa wengine waliosafiri na timu hiyo ni
Kocha Mkuu, Bakari Nyundo Shime maarufu zaidi kwa jina la Mchawi Mweusi,
Daktari wa timu hiyo, Shecky Francis Mngazija na Mtunza Vifaa, Andrew
Vanance Andrew.
Pia yumo Juma Kaseja Juma ambaye kwa muda amechukua nafasi ya makocha
wasaidizi, Sebastian Nkoma na Muharam Mohammed ‘Shilton’ wanaohudhuria
kozi ya makocha ngazi ya juu inayoratibiwa na CAF.
Nyota waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili, Kelvin
Deogratius Kayego na Samwel Edward Brazio wakati mabeki wako Kibwana
Ally Shomari, Nickson Clement Kibabage, Israel Patrick Mwenda, Dickson
Nickson Job, Ally Hussein Msengi, Issa Abdi Makamba na Enrick Vitalis
Nkosi.
Viungo ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali Juma
Ali, Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, Shaban Zuberi
Ada huku washambuliaji wakiwa ni Mohammed Abdallah Rashid, Yohana Oscar
Mkomola na Muhsin Malima Makame.
Serengeti Boys inakwenda kucheza na Afrika Kusini baada ya kuwatoa
Shelisheli kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi zake mbili za kimataifa.
Mshindi wa jumla kati ya Serengeti Boys na Afrika Kusini, atacheza na
timu mshindi kati ya Namibia na Congo-Brazaville.
Hivi karibuni
Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako walishiriki mashindano ya
vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA (AIFF International Youth
Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu
katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki. Ilishika nafasi ya tutu
nyuma ya Korea Kusini na Marekani.#
No comments:
Post a Comment