Mkurugenzi
wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Tanzania Portland Cement Ltd, Simon
Delens akibonyeza kompyuta ili kumpata aliyeibuka mshindi wa droo ya
kwanza ya promosheni
ya “Jijenge na Sementi ya Twiga” iliyofanyika jijini Dar es Salaam
jana, ambapo Mkazi wa Dodoma, Robert Kassim aliibuka mshindi na
kujinyakulia mifuko 600 ya saruji. Wa pili ni Charles Chale wa Dar es
Salaam aliyejipatia mfuko 400 na wa tatu ni Athanas Nyagalu
wa Dodoma mifuko 200. Kushoto walioketi ni Afisa kutoka Bodi ya Michezo
ya Kubahatisha nchini, Bakary Maggid, Mwakilishi wa Bongo Live, Amelye
Chatila (katikati). Mkuu wa Idara ya Promosheni wa Twiga Cement
Martha Haule.
NA KHADIJA KALILI
WASHINDI watatu wa mwanzo wa promosheni ya Jenga na Twiga
Cement wamepatikana leo asubuhi kwenye droo iliyochezesha jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa kwanza ni Robert Kassin (39) kazi yake ni fundi ujenzi ndiye aliyeng’ara
kwenye droo ya kwanza ya Jenga na Twiga Cement
huku akipata zawadi ya mifuko 600 ya Twiga Cement Extra.
Mshindi wa pili ni Charles Chale mwanafuzi wa Chuo Cha
Uhasibu , Mkazi wa Jijini Dar es Salaam amepata zawadi ya mifuko 400 ya Twiga
Extra Cement na nafasi tatu ilikwenda kwa Athanas Nyagalu ambaye pia ni fundi
ujenzi mkaazi wa Chalinze Mkoani Dodoma amepata zawadi ya mifuko 200 ya Twiga Cement
Extra Na yeye ni fundi ujenzi.
Washindi hao walipatana kwenye droo iliyochezeshwa mbele ya
waandishi wa habari na kusimamiwa na Ofisa
wa Bodi ya Bahati Nasibu na kuchezeshwa
na Kampuni ya Bongolive Amelya Chatila.
Akizungumza kabla ya kupatikana kwa wshindi hao kwenye ukumbi uliopo ndani ya Kiwanda cha Wazo
Hill Jijini Dar es Salaam kinachofahamika kwa
jina la Tanzania Portland Cement Company Ltd (TPCC), Mkurugenzi wa Masoko Simon Delens alisema promosheni hiyo inafanyika
kwa kwa mara ya kwanza na amefurahi kuona kwamba zaidi ya wateja 4,000
wameitikia na kushiriki kwa kutuma kuponi
za droo hiyo.
Promosheni hiyo ilizinduliwa inayofahamika kwa jina la ‘Jijenge
Na Twiga Cement’ itadumu kwa majuma nne ilizinduliwa Julai 18 mwaka huu na kilele
chake itakuwa Agosti 28 mwaka huu.
Delens alisema “Twiga Cement inajivunia kuzindua promosheni hii ya
kipekee ambayo inawahusu wateja
wote wa TPCC kwa kupitia promosheni hii
ya ‘Jijenge na Twiga Cement’
washindi watapata nafasi ya kushinda
mifuko 600 ya cement, Kampuni imetenga
jumla ya mifuko 4,800 ya cement
kwa ajili ya promosheni hii”.
Delens aliongeza kwa kusema kuwa Kampuni yao imeamua kuwazawadia
wateja wake waaminifu hivyo
ametoa wito waichangamkie fursa hiyo muhimu huku akizitaja zawadi zingine
zitakazokuwa zikitolewa kwenye promosheni hiyo kuwa ni mashine
za kufyatulia matofali, mixers, matoroli, fulana na kofia.
Delens aliongeza kwa kusema kuwa Kampuni ya Twiga Cement ndiyo inayoongoza kwenye soko
la cement nchini alimalizia kwa
kuwakumbusha na kuwahamasisha wateja wa
Twiga Cement waendelee kununua cement
wanayoitengeneza kwani endapo mteja akipata zawadi ya mifuko itamsaidia
kujenga nyumba.
Akifafanua namna ya kushiri Delens alisema mara baada ya
mteja kununua mfuko wake wa Twiga Extra anaona
namna maalumu ya siri itakayokuwa imewekwa kwenye valvu
ya kila mfuko wa Twiga na
kutakiwa kuituma namba hiyo ya siri kwenda namba 0789 000 666 ambapo atakuwa
ameingia moja kwa moja kwenye droo ya wiki
washindi watakuwa wakipatikana
kila wiki.
No comments:
Post a Comment