Mkurugenzi
wa Msama Action Mart, Alex Msama akionesha waandishi wa habari jijini Dar es
Salaam, stika za TRA pamoja na CD feki ya mwimbaji wa nyimbo za injili Boniphace
Mwaitege wakati wa mkutano na wambayo ni 'feki' lakini imewekwa stika ya TRA.
(Na Mpigapicha Wetu)
NA
MWANDISHI WETU
MKURUGENZI
wa Msama Action Mart ya jijini Dar es Salaam, Alex Msama amewalaumu baadhi ya maofisa
wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhujumu mapato halali ya waimbaji, wasanii
na Serikali.
Msama
alisema jijini Dar es Salaam jana kwamba, baadhi ya maofisa hao wa TRA, wamekuwa
wakiuza ‘stika’ kwa wezi wa kazi wa waimbaji na wasanii ili ‘kutakatisha’ kazi
za wizi.
“Unakamata
CD feki, lakini unakuta ina ‘stika’ ya TRA. Unajiuliza inakuweje? Yote hii ni kutokana na baadhi ya maofisa wa
TRA kuuza ‘stika’ hizi isivyohalali kwa wezi,” alisema huku akionesha mfano wa
stika halali na CD feki.
Msama,
mmoja wa wadau wa vita dhidi ya wizi wa kazi za waimbaji injili na wasanii, alisema
wanachofanya wezi ni kubandika ‘stika’
halali katika kazi feki na kuziuza.
“Hawa
jamaa wamebuni mbinu mpya ya kutumia stika halali za TRA katika kazi feki,
jambo ambalo linahitaji uzoefu kubaini kwamba ni feki,” alisema Msama.
Alisema
hujuma hiyo dhidi ya jasho la waimbaji na wasanii, imekuwa ikiwanyima wahusika
kufaidi jasho la kazi zao kwani huishia kwa wajanja hao wachache.
“Kama si dili ya baadhi ya maofisa wasio waaminifu wa TRA,
wezi hawa wangepata wapi stika hizo? alihoji Msama huku akionyesha stika halali
za
TRA na CD feki.
Alisema
kibaya zaidi ni kwamba, stika hizo feki hazitumiki kwa kazi hizo feki za
waimbaji na wasanii, pia hata kwa bidhaa nyingine ili kuzihalalisha.
Msama
anatoa wito kwa jamii kusaidia vita hiyo ngumu kwa kuacha kununua kazi feki ili
kuinua uchumi wa wasanii na nchi kwa ujumla.
Alisema
vitendo hivyo vya baadhi ya maofisa wasio na uadilifu, vinarudisha nyuma
harakati za Serikali kukusanya mapato kwa ajili ya maendeleo ya nchi.
Msama
ametoa wito kwa uongozi wa TRA kufanya kila uwezalo kuwabaini maofisa hao wenye
kukiuka maadili ya kazi yao
kwani wanakipaka matope chombo hicho.
No comments:
Post a Comment