HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 28, 2016

KIKAO CHA BARAZA KUU CUF CHAFANYIKA ZANZIBAR

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, akisalimiana na viongozi wa chama hicho alipowasili Vuga mjini Zanzibar kwa ajili ya Kikao cha Baraza Kuu la Uongozi ambacho kilikuwa na Ajenda ya tathmini ya mkutano mkuu maalum uliovunjika kutoka na vurugu. (Picha na Talib Ussi).
 Wajumbe wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi (CUF) wakiimba wimbo maalum wa chama hicho ikiwa ni ishara ya kuaza kikao hicho chenye ajenda ya tathmini ya mkutano mkuu maalum uliovunjika wiki iliyopita.


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Kikao cha Siku moja cha Baraza Kuu la Uongozi la CUF kimemalizika na kutoka na maamuzi mazito dhidi ya viongozi na baadhi ya wanachama waliosababisha vurugu katika Mkutano Mkuu Maalum uliofanyika wiki iliyopita.

Kikao hicho ambacho kilifanyika huku jeshi la Polisi likizunguka katika maeneo mengi ya mji wa Zanzibar kiliwashirikisha wajumbe wote kutoka Bara na Visiwani.

Katika kikao hicho kilichofanyika Vuga katika ofisi za Chama hicho walikosekana wajumbe watatu  ambao ni Naibu Katibu Mkuu Bara, Magdelina Sakay, Abdul Kambaya na Masoud ambao inadaiwa walionekana wazi katika kushabikia vurugu ya mkutano wa wiki iliyopita.

Mapema kikao hicho kilipangwa kufanyika katika Hotel Mansonz lakini kwa kile kilichotwajwa hali uasalama ikaaamuliwa kifanyika ofisni hapo.

“Tumefanya maamuzi magumu kuna wengine tayari tumewafukuza na wengine kuwasimamisha” kilisema chanzo chetu kimaja kilichokataaa kutajwa jina lake.

Chanzo kilieleza kuwa hali hakuwa rahisi lakini mwisho wa yoote walifikia maamuzi hayo kwa maslahi ya chama ili kupeleka mapambano mbele katika kudai haki ya ushindi  ya uchaguzi wa Zanzibar uluiofanyika October mwaka jana.

Mkurugenzi wa habari wa chama hicho, Salim Biman  alieleza kuwa hawezi kueleza chochote hadi Agosti 29 saa nne asubuhi ambapo watazungumza na waandishi wa habari ili kuweka hadharani yale yote yaliopitishwa katika kikao hicho.

“Ninacho weza kukwambia kesho tutaongea na waandishi ili tukupeni yoote lakini kwa sasa siko tayari kueleza loloote naomba tukutane kesho” alieleza Biman.

Kikao hicho ambacho kilifanywa katika hali ya tahadhari kilifuatiwa na kikao cha kamati Tendaji na baadae Baraza Kuu.

No comments:

Post a Comment

Pages