2814 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiwapungia wananchi wa Kijiji cha Mtowisa baada ya kuwasili kijijini hapo wakiwa katika ziara ya mkoa wa Rukwa Agosti 24, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wananchi wa kijiji cha Mtowisa mkoani Rukwa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakifurahia ngoma ya asili ya kabila la Wafipa wakati walipowasili kwenye kijiji cha Mtowisa mkoani Rukwa kuzungumza na wananchi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiwapungia wananchi wa kijiji cha Mtowisa baada ya kuwasili kwenye kijiji cha Mtowisa mkoani Rukwa
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Mradi
huo unajengwa kwa usimamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira,
Manispaa ya Sumbawanga (SUWASA), kwa ufadhili wa nchi za Umoja wa Ulaya (EU) na
Serikali ya Ujerumani kupitia benki yake ya Maendeleo (KfW), sh. bilioni 31 utakapokamilika.
Waziri
Mkuu alitoa kauli hiyo jana (Jumatano,
Agosti 24, 2016) wakati na akiweka jiwe la msingi la mradi wa maji safi na
usafi wa mazingira katika Manispaa ya Sumbawanga na kuitaka kampuni ya kampuni
ya Techno Fab Gammon Joint Venture ya India kumaliza ujenzi wa mradi huo haraka
iwezekanavyo.
Alisema
mradi huo ambao tayari umekamilika kwa asilimia 85 unatarajiwa kukamilika
Septemba mwaka huu, hivyo aliwataka wananchi kuhakikisha wanashirikiana na
Manispaa katika kulinda miundombinu ya mradi huo mara utakapokamilika pamoja na
kutunza vyanzo vya maji.
“Pamoja
na Serikali kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maji
inayojengwa katika maeneo mbalimbali nchini,changamoto ya upatikanaji wa huduma
hiyo imekuwa kubwa kutokana na baadhi ya visima vimeanza kukauka hali
inayosababishwa na uharibifu wa mazingira,” alisema.
Alisema
kumekuwa na uvamizi mkubwa katika maeneo ya vyanzo vya maji ambapo wananchi
wanajishughulisha na shughuli za ulimaji, uchungaji wa mifugo, ujenzi wa nyumba
za makazi na uchomaji misitu hivyo kusababisha uchafuzi wa mazingira na
hatimaye vyanzo hivyo hukauka.
Kufuatia
hali hiyo Waziri Mkuu amewaagiza wakuu wote wa wilaya na wenyeviti wa vijiji
nchini kuyasimamia maeneo yenye vyanzo vya maji na kuwaondoa watu
wotewalioyavamia kwa kuwachukulia hatua kali za kisheria pamoja na kuwafikisha
mahakamani.
Naye
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe ambaye alimuwakilisha
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge katika hafla hiyo alisema
aliishukuru Serikali ya Ujerumani na Umoja wa nchi za Ulaya kwa kufadhili mradi
huo.
Hata
hivyo Mhandisi Kamwelwe alisema suala la kuhifadhi mazingira ni msingi endelevu
wa upatikanaji wa maji safi na salama, hivyo aliwaomba wananchi kujiepusha na
uchafuzi wa vyanzo vya maji na uharibifu wa mazingira ili kuepuka athari ya
Taifa kukubwa na janga la ukame.
“Wananchi
wanatakiwa kuacha kufanya shughuli za maendeleo ikiwemo kulima, kufuga ndani ya
mita 60 kutoka katika mito, maziwa na vyanzo vingine vya maji ili kuepusha
uharibifu wa mazingira ambao madhara yake ni makubwa kwa viumbe wote,” alisema.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMIS, AGOSTI 25, 2016.
No comments:
Post a Comment