HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 01, 2016

NSSF YASHIRIKI MAONYESHO YA WAJASIRIAMALI MKOANI MBEYA

  Afisa Masoko na Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Anna Nguzo akisalimia Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Maonyesho ya 13 Wajasiriamali Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yaliyofanyika katika Viwanja vya City Garden jijini Mbeya. PCHA NA KENNETH NGELESI.
 Kaimu Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Mbeya, Yohana Mwambilija, akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla (kulia) alipotembelea banda la shirika hilo wakati wa ufunguzi wa Maonyesho ya 13 ya  Wajasiriamali Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.
Mkaguzi wa NSSF Mkoa wa Mbeya Bupe Mwantole akimkabidhi mwanachama mpya fomu ya kujiunga na NSSF wakati wa maonyesho ya 13 ya wajasiriamali jijini Mbeya.
 Afisa Masoko na Uhusiano wa NSSF,  Anna Nguzo akimkabidhi fomu mwanachama aliyefika katika banda la shirika hilo kwa ajili ya kupata huduma kwenye maonyesho ya 13 ya wajasiriamali  jijini Mbeya.
Mkaguzi wa Shirika la Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Mbeya wa (pili kulia) akimjazia fomu mteja aliyefika kwenye banda la shirika hilo wakati wa maonyesho ya 13 ya wajasiriamali jijini Mbeya. 
Afisa Masoko na Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Anna Nguzo akitoa maelezo kwa watu waliopita katika banda la NSSF wakati wa maonyesho ya SIDO mkoani Mbeya.

No comments:

Post a Comment

Pages