HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 04, 2016

PPF YASAJILI WANAKIJIJI WAJASIRIAMALI 395 KWENYE MPANGO WA WOTE SCHEME IKWIRIRI MKOANI PWANI

 Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele, (kulia), akiwasaidia wanakijiji hawa wa Ikwiriri, Wilayani Rufiji mkoani Pwani, kutuma michango kwa njia ya mtandao wa simu, wakati wa kuandikisha wanachama chini ya mpango wa Wote Scheme kwenye chuo cha Maendeleo ya Jamii, Ikwiriri,  Oktoba 3, 2016. Takriban wanakijiji 395 wakiwemo, wakulima, wafuga nyuki, wavuvi na waendesha bodaboda, wamekabidhiwa kadi za uanachama kupitia mpango huo unaoruhusu mtu yeyote aliye kwenye sekta rasmi na isiyo rasmi kujiunga kwa kuchangia kila mwezi kima cha chini shilingi 20,000.
 Meneja wa PPF, Kanda ya Temeke, Erica Sendegeya, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa Mfuko huo kupitia mpango wa uchangiaji wa Hiari, (Wote Scheme), wakati wa kuandikisha wanachama na kugawa kadi kwenye viwanja vya chuo cha ufundi Ikwiriri, wilayani Rufiji mkoa wa Pwani, Oktoba 3, 2016.
 Zawadi Hamza Sule, (kushoto), ambaye ni mkulima huko Ikwiriri, akipokea kadi yake ya uanachama wa PPF kupitia Wote Scheme

NA MWANDISHI WETU, IKWIRIRI

MFUKO wa Pensheni wa PPF, kupitia mpango wa Uchangiaji wa Hiari, “Wote Scheme”, umesajili karibu wanachama 400  huko Ikwiriri wilayani Rufiji mkoa wa Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi la usajili na ugawaji kadi za uanachama kwenye viwanja vya chuo cha Ufundi Ikwiriri, (IFDC), Oktoba 3, 2016, Meneja wa PPF Kanda ya Temeke, Erica Meshack Sendegeya, alisema,  wanakijiji hao wajasiriamali walihamasika kujiunga na mpango huo baada ya Kanda yake kutoa elimu juu ya umuhimu wa wananchi kujiunga na Mfuko huo kwani kuna manufaa  mengi.

“Tuliwaeleza, mpango huu wa Wote Scheme umebuniwa ili kutoa fursa ya wananchi walioajiriwa au waliojiajiri wenyewe, wakiwemo wakulima, wavuvi, wafugaji, Boda boda  na mama lishe, kujiunga na Mfuko kwa kuchangia kima cha chini cha shilingi 20, 000 kila mwezi. “Fedha hizo unaweza kuzitoa kwa mkupuo au kwa awamu kulingana na uwezo wa mwanachama,” alifafanua Sendegeya.

Akielezea faida za kuwa mwanachama, Meneja huyo alisema, “Mwanachama atafaidika na fao la Afya ambapo atapatiwa bima ya afya kupitia NHIF baada ya kuchangia shilingi elfu 60,000 tu.” Alisema na kuongeza kuwa faida nyingine ni pamoja na mwanachama kujipatia mkopo wa maendeleo ambapo sharti kuu la kupata mkopo huu ni mwanachama kuchangia Mfuko kwa kipindi cha miezi sita, mkopo wa elimu, lakini pia fao la uzeeni, alisema Meneja huyo.

Kuhusu namna mwanachama anavyoweza kuchangia baada ya kujiunga na Mpango huo, Meneja Uhusiano wa PPF, Lulu Mengele alisema, “Kuna njia rahisi ya kuwasilisha michango, ambayo ni kutumia mitandao ya simu, Airtel Money, Tigo Pesa na M-Pesa.” Alisema.

Baadhi ya wanakijiji waliojiunga na Mpango huo, wameipongeza PPF kwa kutoa elimu ambayo imewafanya wajiunge na Mfuko huo na ni matarajio yao utasaidia kuboresha shughuli zao.

“Mimi ni mfuga nyuki, kilichonivutia ni jinsi Mfuko huu unavyoweza kutoa mikopo ya maendeleo,” alisema Erasto Joseph, ambaye pia ni mwalimu wa shule.

Naye Ishara Ibrahim ambaye ni mkulima, alisema, ni matarajio yake kuwa kujiunga na PPF, basi ataweza kumudu kupata huduma ya afya kupitia Bima ya Afya.” Alisema.
  Zawadi Hamza Sule, akionyesha kadi yake baada ya kukabidhiwa
 Seif M. Mgumba akionyesha kadi yake ya uanachama wa PPF, kupitia Wote Scheme
 Khadija R. Kitango, akionyesha kadi yake
 Meneja wa PPF, Kanda ya Temeke, Erica Sendegeya, akizungumza na wanachama hao wapya wa PPF huko Ikwiriri, wilayani Rufiji mkoa wa Pwani Oktoba 3, 2016
 Wanachama wapya wa PPF, wakiwasikiliza viongozi wa PPF 
 Wanachama hawa wapya wakionyeshana kadi zao za uanachama baada ya kukabidhiwa
Wanachama wakisubiri utaratibu wa kukabidhiwa kadi zao na kufanya malipo ya michango ya awali
 Wanachama wapya wa PPF, wakihudumiwa. 
 Meenja wa PPF, Kanda ya Temeke, Erica (kushoto), na Meneja Uhusiano wa Mfuko huo, Lulu Mengele, wakiwasaidia wanachama hao kutumia simu zao za mkononi kuweka michango yao 
 Erica, akiwasaidia kuwaelekeza namna ya kutuma michango kupitia simu za mkononi
 Erica (kulia) na Lulu, wakimsikiliza mwanachama huyu wa Ikwiriri baada ya zoezi la kuwapatia kadi za uanachama Oktoba 3, 2016
 Erica, akisoma majina ya wanachama wapya waliojiunga na PPF kupitia Wote Scheme
 Meneja Uhusiano wa PPF, Lulu Mengele, akiwaarifu waandishi wa habari kuhusu shughuli nzima ilivyokwenda
 Lulu akisalimiana na wanachama hawa wenye furaha
Wanakijiji wa Ikwiriri wakisubiri kupatiwa kadi zao za uanachama baada ya kujiunga na PPF kupitia uchangiaji wa Hiari, (Wote Scheme) Oktoba 3, 2016.

No comments:

Post a Comment

Pages