HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 27, 2016

RAIS MAGUFULI AWATAKA WATANZANIA KUDUMISHA UMOJA 2017

RAIS John Magufuli amewaomba watanzania wote kuulinda, kuutunza na kuudumisha umoja katika mwaka 2017 kwa kufanya kazi kwa bidii.

Rais Magufuli ameandika maombi hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo pamoja na kuwaomba watanzania kutekeleza mambo hayo pia amewatakia heri ya mwaka mpya.

Kupitia ukursa huyo rais aliandika ombi lake kwa watanzania wote waulinde, wautunze na kuudumisha umoja katika mwaka ujao kwa kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii.

“Ombi langu kwa watanzania wote tuulinde, tuutunze na kuudumisha umoja wetu katika mwaka 2017 kwa kufanya kazi kwa bidii. Mungu Ibariki Tanzania,” aliandika rais Magufuli.

Pia aliongeza “Watanzania wenzangu tukiwa tunakaribia kuumaliza mwaka 2016, naomba niwatakie heri ya mwaka mpya 2017,” aliandika.

No comments:

Post a Comment

Pages