HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 12, 2017

YANGA WATUA DAR KILA MCHEZAJI NA NJIA YAKE

Wachezaji Haji Mwinyi (kushoto) na Juma Mahadhi wakipatana bei na waendesha bodaboda wakati walipowasili katika bandari ya Dar es Salaam jana, wakitokea Zanzibar katika mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi dhidi ya Simba ambapo walifungwa kwa penalt 4-2. (Picha na Francis Dande).
Beki wa Yanga, Haji Mwinyi akiwa amepanda bodaboda mara baada ya kuwasili katika bandari ya Dar es Salaam, wakati kikosi hicho kikitokea Zanzibar katika mashindano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kutolewa na Simba katika hatua ya Nusu Fainali ya michuano hiyo.
 Mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe akielekea kutafuta usafiri.
 Kocha Mkuu wa Yanga, George Lwandamila. 
  Mashabiki wa soka wakimzonga kocha wa makipa wa Yanga, Juma Pondamali.
 Shabiki wa Simba akimzodoa Kocha wa Makipa wa Yanga, Juma Pondamali.
 Dida akiwasili.
 Kipa wa Yanga, Deogratius Munishi 'Dida' akipanda basi la timu hiyo baada ya kuwasili wakitokea Zanzibar katika kombe la Mapinduzi.

No comments:

Post a Comment

Pages