HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 22, 2017

WAZIRI NAPE APOKEA RIPOTI YA UCHUNGUZI WA KUVAMIWA KWA OFISI ZA CLOUDS MEDIA

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa ripoti ya Kamati ya watu wa tano aliyounda kufanya Uchunguzi wa tukio la Uvamizi wa Kituo cha Televisheni cha Clouds lililofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. (Picha na Said Powa).

Mwenyekiti wa Kamati iliyoundwa kuchunguza tukio la Uvamizi wa Ofisi za Clouds Media, Dk. Hassan Abbas, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi ripoti hiyo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, akipokea ripoti ya Kamati ya watu wa tano, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dk. Hassan Abbas, iliyoundwa kufanya Uchunguzi wa tukio la Uvamizi wa Ofisi za Clouds Media lililofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, mwishoni mwa wiki iliyopita.

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, baada ya kukabidhiwa ripoti hiyo.

No comments:

Post a Comment

Pages