HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 14, 2017

KAMPUNI YA BIN SLUM YAKABIDHI MSAADA WA MATAIRI 12 KWA HUDSON KAMOGA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MBULU MKOANI MANYARA

1
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga kulia akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wa kampuni ya Bin Slum kwa mchango wake katika maendeleo ya wilaya ya Mbulu baada ya kampuni hiyo kupitia kwa meneja Mauzo wake Bw. Salum Aljabiry kumkabidhi moja ya matairi 12 ya magari madogo kutoka kwa Kampuni ya hiyo jijini Dar es salaam .Kampuni ya Bin Slum imetoa msaada huo kwa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu ili kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Pombe Magufuli.
2
Mkurugenzi wa Harmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga kulia akipokea moja ya matairi 12 ya magari madogo kutoka kwa, Salim Aljabiry, Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bin Slum .Kampuni hiyo imetoa msaada huo kwa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu ili kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Pombe Magufuli.
5
Baadhi ya matairi yanayouzwa na kampuni ya Bin Slum Chang'ombe jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages