HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 08, 2017

KONGAMANO LA WILDAF LA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

 Mkurugenzi wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WILDAF), Dk Judith Odunga akizungumza na washiriki wa kongamano la Siku ya Wanawake Duniani lililofanyika Dar es Salaam. Kusoto kwake ni Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Umma kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Justus Mulokozi, Mwenyekiti wa shirika hilo, Naomi Kaihula (wa pili kulia) na wajumbe wengine wa shirika hilo.
Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Umma kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Justus Mulokozi akizungumza na washiriki wa kongamano la Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WILDAF) na kufanyika Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WILDAF, Naomi Kaihula akizungumza na washiriki wa kongamano la Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na shirika hilo na kufanyika Dar es Salaam.
 Wasanii wa kikundi cha ngoma cha Nimujo wakiburudisha wakati wa kongamano hilo.
Wadau na washiriki wa kongamano la Siku ya Wanawake duniani lililoandaliwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WILDAF).
 Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Umma kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Justus Mulokozi akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika (WILDAF) Naomi Kaihura (kushoto kwake), Mkurugenzi wa shirika hilo, Dk Judith Odunga (kulia kwake) na wajumbe wa shirika hilo wakati wa kongamano la Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na Shirika hilo na kufanyika Dar es Salaam.
Washiriki wa kongamano la Siku ya Wanawake duniani lililoandaliwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WILDAF) wakifuatilia matukio ya kongamano hilo Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages