Kocha Mkuu wa timu ya mpira
wa miguu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Mayanga (pichani), leo Jumatatu Machi 13, 2017
ametangaza majina ya wachezaji 26 watakaounda kikosi hicho.
Taifa Stars, inatarajiwa
kucheza na Botswana Machi 25, 2017 kabla ya kuivaa Burundi Machi 28, mwaka huu
katika michezo kirafiki wakati huu wa Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la
Mpira wa Miguu (FIFA).
Katika mkutano wake na
wanahabari uliofanyika leo Makao Makuu ya TFF, yalioko Uwanja wa Karume, Ilala
jijini Dar es Salaam, Mayanga aliwataja wachezaji hao kuwa ni walinda milango, Aishi
Manula (Azam FC), Deogratius Munishi (Yanga
SC) na Said Mohammed (Mtibwa Sugar).
Walinzi wa pembeni upande
wa kulia aliwataja Shomari Kapombe (Azam
FC) na Hassan Kessy (Yanga SC) wakati upande wa kushoto wapo Mohammed Hussein
(Simba) na Gadiel Michael (Azam FC).
Mayanga aliwataja walinzi
wa kati Vicent Andrew (Yanga SC), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba
SC) na Erasto Nyoni (Azam FC) ilihali
aliwataja viungo wa kuzuia kuwa ni Himid Mao (Azam
FC) na Jonas Mkude (Simba SC).
Kadhalika wako viungo wa kushambulia
Salum Abubakar (Azam FC), Said Ndemla (Simba
SC), Frank Domoyo (Azam FC) na Muzamil Yassin (Simba) wakati viungo wa kulia
waliotajwa ni Simon Msuva (Yanga SC) na Shizza
Kichuya (Simba SC).
Viungo wa kushoto ni Farid Mussa (Teneriffe, Hispania) na Hassan Kabunda (Mwadui FC) wakati washambuliaji ni Mbwana
Samatta (KRC Genk- Ubelgiji), Thomas
Ulimwengu na AFC Eskilstuna – Sweden), Ibrahim
Ajib (Simba SC), Mbaraka Yusufu(Kagera Sugar) na Abdul-Rahman Mussa (Ruvu
Shooting).
Pia Mayanga aliwataja
wasaidizi wake kuwa Kocha Wa Makipa, Patrick Mwangata wakati Meneja wa timu
upande wa ufundi atakuwa mwenyewe Mayanga na upande wa mipango mingine atakuwa Danny
Msangi; Mtunza Vifaa, Ally Ruvu wakati Daktari wa timuatakuwa Richard Yomba
huku Daktari wa viungo akiwa ni Gilbert
Kigadya.
Timu hiyo itaingia kambini Machi
19, 2017 kwenye Hoteli ya Urban Rose, Dar es Salaam na mara baada ya michezo
hiyo kambi itaahirishwa Machi 29, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment