FIKIRI KAPINGA, MBINGA
Mtawa mmoja wa kanisa katoriki jimbo la mbinga mkoani Ruvuma amefikishwa katika mahakama ya wilaya kujibu tuhuma za uwizi wa Fedha jumla ya TSHS.M.28.8/= mali ya Jimbo .
Imedaiwa na mwendesha mashtaka wa Polisi Ast Inspekta SEIF KILUGWE mbele ya hakimu mkazi mfawidhi katika mahakama ya wilaya mbinga MAGDARENA NTANDU kuwa mtuhumiwa Mtawa EMANUELA NINDI [40] wa kanisa katoriki Jimbo la mbinga amedaiwa kutenda makosa hayo mwaka jana kwa nyakati tofauti tofauti akiwa mtunza fedha za Jimbo hilo .
KILUGWE aliendelea kudai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa EMANUELA alikuwa anachukua Fedha hizo kidogo kidogo hadi kufikia jumla ya TSHS .M. 28.8/= ambazo ni makusanyo ya miradi mbali mbali ya Jimbo pamoja na michango ya waumini .
Mshtakiwa alikana mashtaka na yuko mahabusu kwa kukosa wadhamini wawili wenye sifa hadi machi 28 mwaka huu kesi hiyo itakapo tajwa tena
No comments:
Post a Comment