Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu wa Tigo, Ruan Swanapoel, akizungumza katika uzinduzi wa huduma ya BimaMkononi. Kushoto ni Meneja wa Milvik Tanzania, Tom Chaplin.
Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu wa Tigo, Ruan Swanapoel, akizungumza katika uzinduzi wa huduma ya BimaMkononi.
Meneja wa Milvik Tanzania, Tom Chaplin, akifafanua jambo katika uzinduzi wa bima ya afya ya BimaMkononi.
Mmoja wa wanufaika wa huduma ya bima ya afya ya BimaMkononi akizungumza.
Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu wa Tigo, Ruan Swanapoel, wakati wa uzinduzi wa BimaMkononi uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu wa Tigo, Ruan Swanapoel, akizungumza katika uzinduzi wa huduma ya BimaMkononi.
Meneja wa Milvik Tanzania, Tom Chaplin, akifafanua jambo katika uzinduzi wa bima ya afya ya BimaMkononi.
Mmoja wa wanufaika wa huduma ya bima ya afya ya BimaMkononi akizungumza.
Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu wa Tigo, Ruan Swanapoel, wakati wa uzinduzi wa BimaMkononi uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mnufaika wa Huduma ya Bima ya Afya inayotolewa na kampuni ya Tigo, Hawa Ramadhan akitoa maelezo ya namna alivyonufaika na huduma hiyo wakati wa uzinduzi wa Bima Mkononi uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu wa Tigo, Ruan Swanapoel. (Picha na Francis Dande).
NA MWANDISHI WETU
KAMPUNI ya Milvik inayoongoza kwa bima ndogo nchini kwa
kutumia teknolojia ya simu za mkononi katika kutoa huduma za bima ya afya, imejipanga
kuleta mageuazi makubwa katika sekta ya ndani ya bima
kupitia mfumo wa TigoPesa.
Kampuni ya Tigo kwa kushirikiana na kampuni Milvik, zimeingia
makubaliano ya kutoa Huduma hiyo tangu mwaka jana kwa kutoa Huduma ya bima kwa
simu za mkononi maarufu kama Bima Mkononi inayotoa bidhaa za kipekee.
Bidhaa hizo za hali ya juu, ni kama bima ya maisha, ugonjwa
na ajali kwa wateja wanaotumia Huduma ya TigoPesa, ikiwa na wateja hai zaidi ya
200,000.
Hawa Ramadhani, mama wa watoto watatu kutoka wilaya ya Kibaha, mkoa wa Pwani, ni mmoja wa wanufaika wa BimaMkononi anaeleza
mengi kuhusu manufaa ya program hiyo katika kusaidia wananchi kupitia
Tigopesa.
Akieleza jinsi BimaMkononi
ilivyobadilisha maisha yake, anasema: “Nilikuwa nimelazwa katika
Hospitali ya Tumbi kwa siku 21, baada ya kuruhusiwa kutoka, niliwasilisha taarifa za hospitali katika duka la Tigo la
huduma kwa wateja na nilifurahi waliponiita baada ya siku tatu na kupokea
kitita cha 840,000/-
Alisema, baada ya
kuitwa alielezwa kuwa bima imemfidia kwa
kipindi alichokuwa amelazwa hospitalini.
“Kwa pesa hizo niliweza
kulipia ada ya shule ya watoto iliyokuwa imebaki, pamoja na kukuza biashara yangu ndogo,” alisema na kutoa
ushauri kwa wengine kujiunga na mpango
huo ili wafurahie manufaa yake.
Naye Melikizedeki Nyalufujo, mwanafunzi wa mwaka wa tatu
Chuo Kikuu cha Uhandisi na Teknolojia cha St. John, Dar es Salaam, alisema anajisikia furaha kuwa
mnufaika wa BimaMkononi, baada ya kupokea 86,000/- kufuatia kulazwa kwake
hospitalini kwa siku mbili kutokana na jeraha alilolipata.
“Mara ya kwanza nilipoelezwa kuhusu BimaMkononi nilikuwa na
wasiwasi, lakini nilijiunga. Hata hivyo, nilishawishika kujiunga baada ya
kupokea fedha hizo ndipo nilithibitisha
kwamba ilikuwa ni kweli.
“Ankara za hospitali
ilikuwa ni 16,000/-; hivyo kwa fedha
hii ya ziada niliweza kulipia gharama nyingine kama vile kujikimu chuoni, kununia vifaa vya masomo na kulipia baadhi ya madeni madogo
ambayo nilikuwa nimekopa hapo awali.
Naishukuru mno BimaMkononi,” alisema Nyalufujo kwa furaha.
Kwa mujibu wa Meneja wa Milvik Tanzania, Tom Chaplin, huduma
ya BimaMkononi imetengenezwa makusudi kutoa bidhaa za Bima kwa Watanzania wote
ambao wanaihitaji ambao kinyume cha
hapo, wasingeweza kumudu huduma hiyo.
BimaMkononi, ni mfumo mpya wa bima kwa Watanzania wa kawaida
ambayo inawawezesha kuwakinga dhidi ya matukio yasiyotarajiwa yanayoweza kuwa
na athari kwa hali ya kifedha kama wasingekuwa wamejiunga na huduma hiyo. Tayari BimaMkononi ishalipa fidia ya zaidi ya
shilingi milioni 27 katika miezi sita iliyopita.
No comments:
Post a Comment