Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO Dkt Hassan Abbas akichangia jambo wakati wa kikao cha 12 cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali kinachofanyika Mkoani Dodoma.
Maafisa Mawasiliano wa Serikali kutoka Wizara,Taasisi, Halmashauri,Wakala na Mashirika ya Umma,Tamisemi na Idara zinazojitegemea wakimskiliza kwa makini Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye (hayupo Pichani) wakati akifungua Kikao kazi cha 12 cha Maafisa hao kinachofanyika Mkoani Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Bahi Bi.Elizabeth Kitundu akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao kazi cha 12 cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali kinachofanyika Mkoani Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bi.Nuru Milao akiongea kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye kufungua rasmi Kikao kazi cha 12 cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali kinachofanyika Mkoani Dodoma tarehe 14 Machi 2017.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akizungumza na Maafisa Mawasiliano wa Serikali wakati akifungua kikao kazi cha 12 cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali kinachofanyika Mkoani Dodoma.
Mwenyekiti
wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini
(TAGCO) akichangia jambo wakati wa Kikao kazi cha 12 cha Maafisa Mawasiliano wa
Serikali kinachofanyika Mkoani Dodoma.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa Kikao kazi cha 12 cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali kinachofanyika Mkoani Dodoma.Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi.Nuru Milao,Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi Bi.Elizabeth Kitundu,Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Dkt.Hassana Abbas na Mwenyekiti wa TAGCO Bw.Innocent Mungy.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Mawasiliano kutoka Idara ya Habari-MAELEZO wakati wa kikao cha 12 cha Maafisa hao wa Serikali kinachofanyika Mkoani Dodoma. Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi.Nuru Milao,Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi Bi.Elizabeth Kitundu,Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Dkt.Hassana Abbas na Mwenyekiti wa TAGCO Bw.Innocent Mungy.
Na:
Lorietha Laurence – WHUSM, Dodoma
Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amewataka Maafisa Habari,
Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kuzisoma, kuzielewa na kuzifanyia kazi
sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 na ile ya Haki ya kupata Taarifa ya mwaka 2016 ili kuweza kutekeleza majukumu
yao kwa ufanisi katika kuuhabarisha umma.
Waziri
Nape ameyasema hayo leo Mjini Dodoma alipokuwa akifungua mkutano wa Maafisa
Mawasiliano Serikalini ambapo licha ya kuwataka kuzijua sheria hizo pia
amewataka kuwa wabunifu kuendana na maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia katika
utendaji kazi wa kila siku.
Aidha
aliongeza kuwa kuwepo kwa sheria hizo mbili kutatengeneza daraja
litakalounganisha na kuwezesha utekelezaji wa majukumu ya Serikali kwa wananchi.
“Ni wajibu
wa Maafisa Mawasiliano kuzijua na kuzitendea kazi sheria hizi ili kurahisisha
upatikanaji wa mawasiliano baina ya serikalini na umma hivyo kuondoa ugumu
uliokuwepo hususani katika kupatikana kwa taarifa muhimu kwa wananchi” alisema Waziri
Nape.
Aliongeza
kwa kufafanua kuwa endapo utekelezaji wa sheria hizi mbili muhimu utasimamiwa
na kuzingatiwa basi kutakuwepo na matokeo chanya ya kiutendaji na hivyo kuleta
mafanikio makubwa yanayotarajiwa na umma.
Waziri
Nape pia aliwataka Maafisa Mawasiliano hao kuwa wabunifu katika utekelezaji wa
majukumu yao kwa kuendana na maendeleo ya teknolojia ikiwemo matumizi ya
mitandao ya kijamii katika kuhabarisha umma na kutoa taarifa kwa wakati.
“Zama hizi
sio zile za maafisa mawasiliano kujisifia kwa kuwa na safari nyingi badala yake
kuwa watekelezaji wa kazi zao kwa wakati na matokeo yanayoonekana kwa umma ila
kwa atakayeshindwa kutekeleza hayo basi tutaomba atupishe” alisema
Waziri Nape.
Aidha
alieleza kuwa anafahamu kuwa kuna changamoto nyingi ambazo maafisa mawasiliano
wanakumbana nazo katika utendaji wao wa kazi ikiwemo ukosefu wa vifaa ingawa si
kigezo cha wao kutokutekeleza wajibu wao.
Katika
kuhakikisha kuwa changamoto ya ukosefu wa vifaa inatatuliwa Waziri Nape alitoa
Wito kwa Makatibu Wakuu, Wakurugenzi na Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuweka
kipaumbele katika bajeti hii mpya kwa kutenga kiasi cha fedha ambacho kitasaidia
kununua vifaa kwa ajili ya Maafisa Mawasiliano wa Wizara, Taasisi, Mikoa,
Wilaya na Halmashauri.
Naye Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao
alisema kuwa umuhimu wa mkutano wa Maafisa Mawasiliano Serikalini ni katika
kuwajengea uwezo wa kiutendaji pamoja na kutathmini utendaji kazi wao.
Kwa upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Elizabeth Simon Kitundu ameishukuru
Wizara kuandaa mafunzo kwa Maafisa Mawasiliano Serikalini na kuyafanyia Mkoani
Dodoma kwani kwa kufanya hivyo itarahishisha mfumo wa kimawasiliano na
kutangaza fursa zilizopo Mkoani Dodoma hivyo kuwafanya watumishi wa umma kuwa na
amani katika kutekeleza agizo la kuhamia Dodoma.
Mkutano wa
Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini umefanyika kwa mara ya 12
huku lengo ikiwa ni kuwakutanisha kwa pamoja maafisa hao kutoka katika ngazi
mbalimbali za kiutendaji serikalini ikiwemo Wizara, Idara, Taasisi, Mikoa,
Wilaya na Halmashauri ili kuweza kubadilishana uzoefu wa kiutendaji pamoja na
kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.
No comments:
Post a Comment