HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 15, 2017

RAIS MAGUFULI AZINDUA MABWENI YA WANAFUNZI UDSM, AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA NYUMBA ZA WAKAZI WA MAGOMENI KOTA

Rais John Magufuli akizungumza katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za Wakazi wa Magomeni Kota jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande).
 Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia akizungiumza katika hafla ya kuweka jiwe la Msingi la Nyumba za Wakazi wa Magomeni Kota jijini Dar es Salaam. 
 Rais Magufuli akikagua ujenzi wa Nyumba za Wakazi wa Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.
  Rais Magufuli akikagua ujenzi wa Nyumba za Wakazi wa Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.
  Rais Magufuli akikagua ujenzi wa Nyumba za Wakazi wa Magomeni Kota jijini Dar es Salaam. 
 Rais Magufuli akisalimiana na msanii wa Bongo Movie, Mahsin Awadh 'Dk. Cheni'.  
 Rais Magufuli akiwasalimia wananchi.
 Rais Magufuli akipiga tumba wakati bendi ya Msondo Ngoma ikitumbuiza katika hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa nyumba za wakazi wa Magomeni Kota.
 Rais Magufuli akipiga tumba wakati bendi ya Msondo Ngoma ikitumbuiza katika hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa nyumba za wakazi wa Magomeni Kota. 
 Rais Magufuli akipiga tumba wakati bendi ya Msondo Ngoma ikitumbuiza katika hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa nyumba za wakazi wa Magomeni Kota. 
 Rais John Magufuli akiwapungia mkono wananchi. 
  Rais Magufuli akimshika mkono Bi. Mwajuma Khamis Sama (70) ambaye ni mmoja kati ya wakazi 644 wa Magomeni Kota ambao watanufaika na mradai wa ujenzi wa nyumba hizo.
 Wananchi wakiwa na shauku ya kutaka kumsalimia Rais.
 Baadhi ya wadau waliojitokeza katika uzinduzi wa mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Wasanii kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakitumbuiza.
Sehemu ya mabweni 20 yenye uwezo wa kupokea wanafunzi 3840 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo Rais John Magufuli ameyazindua leo. 
Sehemu ya mabweni 20 yenye uwezo wa kupokea wanafunzi 3840 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo Rais John Magufuli ameyazindua leo.   
  Sehemu ya mabweni 20 yenye uwezo wa kupokea wanafunzi 3840 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo Rais John Magufuli ameyazindua leo. 
 Sehemu ya mabweni 20 yenye uwezo wa kupokea wanafunzi 3840 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo Rais John Magufuli ameyazindua leo.  
  Sehemu ya mabweni 20 yenye uwezo wa kupokea wanafunzi 3840 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo Rais John Magufuli ameyazindua leo. 
  Sehemu ya mabweni 20 yenye uwezo wa kupokea wanafunzi 3840 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo Rais John Magufuli ameyazindua leo. 
  ehemu ya mabweni 20 yenye uwezo wa kupokea wanafunzi 3840 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo Rais John Magufuli ameyazindua leo. 
 Makatibu Wakuu waliohudhuria hafla hiyo.
 Makada wa CCM pamoja na wananchi waliohidhuria hafla hiyo.
 Wananchi wakiwa katika hafla hiyo.
Wadau mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo.
 Rais John Magufuli akizundua rasmi mabweni 20 ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere-Mlimani, ambapo jumla ya wanafunzi 3840 watanufaika ujenzi wa mabweni hayo. 
 Rais John Magufuli akizundua mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwl Julius Nyerere-Mlimani. 
  Rais John Magufuli akizundua mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwl Julius Nyerere-Mlimani.
  Rais John Magufuli akizundua mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere-Mlimani.
  Rais John Magufuli akizundua mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwl Julius Nyerere-Mlimani.
  Rais John Magufuli akizindua rasmi mabweni 20 ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). 
  Rais John Magufuli akizundua mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere-Mlimani.
  Rais John Magufuli akikata utepe  wakati wa uzinduzi rasmi wa mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere-Mlimani.
Rais John Magufuli akikata utepe  wakati wa uzinduzi rasmi wa mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere-Mlimani.

 Kikundi cha ngoma kikitumbuiza.
 Ngoma.
 Rais John Magufuli akikata utepe  na Bi. Mwajuma Khamis Sama (70) ambaye ni mwakilishi wa wakazi 644 wa Magomeni Kota ambao watanufaika na mradai wa ujenzi wa nyumba hizo.
 Rais John Magufuli akiweka jiwe la msingi kata utepe  na Bi. Mwajuma Khamis Sama (70) ambaye ni mwakilishi wa wakazi 644 wa Magomeni Kota ambao watanufaika na mradai wa ujenzi wa nyumba hizo.
Rais Magufuli Aagiza TCU kutowachagulia Wanafunzi wa Elimu ya Juu Vyuo.


Na: Lilian Lundo na Beatrice Lyimo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kutowachagulia vyuo wanafunzi wa elimu ya juu na kuwaacha wanafunzi hao kuchagua vyuo wanavyovitaka wenyewe.
Agizo hilo limetolewa leo, Jijini Dar es Salaam Rais Magufuli alipokuwa akizindua Mabweni mapya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa Chuoni hapo Juni, mwaka jana.
“Ninaamini kama wanafunzi wangepewa nafasi ya kuchagua vyuo wanavyovipenda wenyewe, vyuo vya Serikali kama vile Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kikuu cha Mzumbe vingekuwa na wanafunzi wengi sana,” alisema Dkt. Magufuli.
Aliendelea kwa kusema kuwa TCU imekuwa ikiwachagulia wanafunzi vyuo visivyo na sifa na makazi ya wanafunzi hivyo kusababisha wanafunzi hao kusoma katika mazingira magumu na wanapomaliza masomo yao hukosa ajira kutokana na vyuo hivyo kutokuwa na sifa.
Aidha, Rais Magufuli ameuagiza uongozi wa UDSM kutoza wanafunzi gharama ya shilingi mia tano(500) kama malipo ya makazi ya  mabweni hayo kwa siku badala ya shilingi mia nane(800) inayotozwa kwa mabweni mengine yaliyopo chuoni hapo.
Alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuwekeza katika elimu hivyo itahakikisha wanafunzi nchini wananufaika kwa kupata elimu bora kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu.
“watanzania walinichagua ili kutatua changamoto zinazowakabili na hivi ndivyo ninavyofanya kutatua changamoto hizo” alisema Rais Magufuli.
Naye, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amempongeza Rais Magufuli kwa kutoa shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni hayo ambao kwa kiasi kikubwa yatatatua changamoto ya makazi iliyokuwa ikiwakabili wanafunzi wa chuo hicho.
Prof. Ndalichako amesema kuwa mabweni hayo yamejengwa kwa kipindi cha miezi 8 ambayo yatachukua wanafunzi 3840.
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Rwekaza Mukandala ametoa rai kwa wanafunzi wa chuo hicho kuhakikisha wanaimarisha usalama katika maeneo ya mabweni hayo na kulinda miundo mbinu yote iliyoweka.
“Ni lazima mzingatie matumizi sahihi ya kila kifaa kilichofungwa katika majengo haya, majengo haya ni mapya na yamejengwa kwa gharama kubwa kwa lengo la kutusaidia kuondokana na changamato iliyotukabili kwa muda mrefu,” alisema Prof. Mukangala.
Wakati huohuo Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi magomeni “QUARTERS”, mradi ambao kwa asilimia kubwa unawagusa watanzania wa hali ya chini.
Aidha Rais Magufuli ameendelea kusisitiza juu ya ahadi aliyoitoa kwa wakazi 644 waliokuwa wakiishi maeneo hayo kupewa nyumba ambapo wataishi bure kwa muda wa miaka mitano.
Pia, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo (TBA) Msanifu Majengo Elvis Mwakalinga amesema ujenzi wa mradi huo umezingatia miundombinu yote iliyohitajika ambapo itakuwa na sehemu za makazi, biashara, maegesho ya magari na bustani ya kupumzikia.
Ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja ambapo ujenzi wake ulianza rasmi Octoba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

Pages