HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 15, 2017

TAARIFA KWA WAKANDARASI WANAOTEKELEZA MIRADI YA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatambua kuwa baadhi ya wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kusambaza umeme vijijini hawajakamilisha miradi kwa mujibu wa MIKATABA waliyosaini na Wakala (REA). Aidha, kuna baadhi ya wakandarasi wamekamilisha miradi lakini hawajakabidhi rasmi miradi hiyo na vifaa au hawajafanya marekebisho kasoro zilizobainishwa na wasimamizi wa miradi kutoka (TANESCO na REA).

Kwa tangazo hili, Wakala unawataarifu wakandarasi wote ambao hawajakamilisha matakwa hayo ya kimikataba kufanya hivyo mara moja. Wakandarasi watakaoshindwa kutimiza masharti hayo hawataruhusiwa kushiriki katika zabuni zitakazotangazwa na Wakala (REA) baada ya TANGAZO hili na hatua nyingine zitachukuliwa juu yao kwa mujibu wa mikataba hiyo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la Mawasiliano, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma, 14414
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

No comments:

Post a Comment

Pages