HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 05, 2017

Uchukuzi yaadhimisha siku ya Mazingira NIT

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi), Dk. Leonard Chamuriho aliyekuwa Mgeni rasmi akiwahutubia wafanyakazi wa taasisi zilizopo chini ya sekta hiyo, kabla ya kuanza kwa zoezi la kufanya usafi wa mazingira kwenye Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT) na Soko la Mabibo, ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani iliyoadhimishwa jana.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi), Dr. Leonard Chamuriho akimwagilia maji mti aliopanda ndani ya Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT), ikiwa ni moja ya kazi zilizofanyika jana kwenye kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, iliadhimishwa kwa kufanyika usafi maeneo ya nje ya chuo hicho na soko la Mabibo. 
Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege vya Mikoa (DRA), Bw. Valentine Kadeha (katikati) akishirikiana kupanda mti na wanafunzi wa shule ya Mpakani ya Mabibo, katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, iliyoadhimishwa jana kwa wafanyakazi wa taasisi mbalimbali wa Sekta ya Uchukuzi kufanya usafi nje ya Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT) na Soko la Mabibo.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakiungana na wenzao kutoka taasisi mbalimbali za Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi) jana kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira kwenye Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT) na Soko la Mabibo ikiwa jana ni Siku ya Mazingira Duniani. 
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakifagia nje ya uzio wa Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT), ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani iliyofanyika jana kwa kusafishwa mazingira hayo na ndani ya soko la Mabibo. 

No comments:

Post a Comment

Pages