HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 24, 2017

JPM Mgeni Rasmi ‘ALAT’ Taifa

NA KENNETH NGELESI,MBEYA

RAIS  wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuri, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika Mkutano wa Mkuu Taifa wa Jumuhiya ya Serikali ya Mitaa wa, ALAT, ambao kitaifa utafanyika Jijini Mbeya, kuanzia Agosti 19 hadi 22, mwaka huu.

Mkutano huo ambao utafanyika katika Ukimbi wa Mkapa,ni wa 33 na kwamba unatarajia kukutanisha wajumbe zaidi ya 800 wa ndani ya nchi pamoja na wadau mbalimbali kutoka nje ya nchi.

Taarifa ya Mkutano huo ilitolewa jana  kwa waandishi wa habari jijini hapa na , Makamu Mwenyekiti ALAT Taifa, Stephen Mhapa baada ya kumaliza kutembelea na kukagua eneo litakalofanyika mkutano huo.

Akizungumza na waandishi Mhapa alisema kuwa Mkutano huo, unafanyika Mbeya kutokana na ombi maalum lililoombwa na Meya wa Jiji la Mbeya, David Mwashilindi kwa kushirikiana na wenyeviti wa halmashauri kutokana na changamoto za kimamlaka zinazozikabili halmashauri hizo katika utendaji kazi.

Alisema mkutano huo ni fursa kwa wakazi wa jiji la mbeya na halmaashuri waone ni nimna gani wanaweza kuzitumia ugeni unaeweza kuwanufaiasha.

 ‘ALAT Kama tunavyofahamu kazi kubwa ya ALAT ni kuhakikisha inatoa elimu kwa wajumbe wake ili wafahamu mipaka ya madaraka na ya kiutendaji lengo likiwa ni kupunguza au kutokomeza migogoro isiyo ya lazima inayozikumba halmashauri,”alisema.

Aidha, alisema kuwa mkutano huo, Rais Magufuli ataambana na viongozi akiwemo waziri mwenye dhamani na wizara hiyo pamoja na katibu Mkuu lakini pia pia utashirikisha nchi wanachama wa Jumuhiya ya Afrika Mashariki kutoka nchi ya Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Akizungumzia Mkutano huo, Meya wa Jiji la Mbeya, Mwashilindi, aliwataka wananchi wa Mkoa wa Mbeya, kuhakikisha wanatumia fursa hiyo katika kukuza uchumi pamoja na kutangaza bidhaa mbalimbali zinazozalishwa ndani ya eneo hilo.

“Tumepokea kwa mikono miwili jukumu la kuaandaa mkutano huu, na sisi kama Jiji tupo vizuri na tunaendelea na maandalizi kwani hata uongozi ALAT, Taifa wameridhika na mahali patakapo fanyika Mkutano,”alisema.

Hata hivyo, alisema mkutano huo ni fursa kwa wajumbe mbalimbali hasa Madiwani ili kufahamu namna ya uendeshaji wa halmashauri na kufahamu mipaka ya majukumu yao ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Alat Mkoa wa Mbeya Mwalego Chisengo alisema kuwa Mkutano una manufaa kwa wananchi wa Mkoa Mbeya hivyo ni fursa Pekee kwa wananchi kutumia.

‘Mkutano huu ni fursa kwa wananchi hasa katika eneo la Uchumi hakuna asiye fahamu kuwa Mbeya tunazalisha vyakula hivyo uwepo wa wageni ni fursa na wajibu wetu kuitumia kwani wageni hawa watakuja na fedha tutauza vyakula lakini pia watalala kwenye nyumba zetu za kulala wageni’ alisema Chisengo

No comments:

Post a Comment

Pages