HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 23, 2017

Wakulima wa zao la mwani walia na bei pamoja na kodi

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, akipata maelezo ya jinsi ya matumizi ya mwani na faida zake kutoka kwa mkulima wa zao hilo, Bi Mariam Pandu Kweleza katika Kijiji cha Bwejuu mjini Zanzibar. (Picha na Talib Ussi).
Bi Mariam akimwonyesha Balozi Seif  mfano wa shamba la mwani na jinsi mwani unavyolimwa.

Na Talib Ussi, Zanzibar

Wakulima na Wauzaji wa mwani Zanzibar wamelalamika   kodi kubwa  wanazotozwa Katika ngazi tofauti za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na bei  ndogo kwa zao hilo kwa madai kuwa haiendani na gharama za kilimo hicho.

Kilio hicho wamekitoa katika maadhimisho ya siku ya Mwani Zanzibar ambayo imeandaliwa na tasisi ya Milele Zanzibar Foundation mbele ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif  Ali Iddi wakati akigagua bidhaa zinazlishwa kutokana mwani.

Mariam Pandu Kweleza mkulima wa mwani kutoka Kijiji cha Bwejuu, alimuambia kiongozi huyo mkuu wa serikali ya Mapinduzi  Zanzibar kuwa kazi wanayofanya ni ngumu  na huku pato wanalolipata si robo ya maumivu ukulima wa kilimo hicho.

“Mheshimiwa kilo 300, kweli zitaweza kufuta jasho letu kwani kazi hii ni ngumu mnoo na sasa hivi tuambiwa ni zao la tatu kwa kuingiza fedha za kigeni lakini wakulima bado tunaumiaa” alilalamika bi Mariam.

Alieleza kuwa bei ya biashara yao hiyo inapangwa na makampuni bila kuangalia kazi ngumu zinazo fanywa na wakulima hao ambao wengi wao ni wanawake tena wajane.
Amina Khamis muuzaji wa bidhaa zinazotokana na zao la mwani alieelza kuwa makato wanayokatwa ni makubwa kupitia taasisi mbili tofauti kubwa ikiwemo TRA na ZRB.

Alimuomba kiongozi huyo kuwa kuna haja ya kuziangalia upya kodi wanazokatwa ili wawe kufanyakazi yenye manufaa kwa wakulima Pamoja na Serikali kwa ujumla.

Akizungumzi katika ghafla ya ufunguzi wa siku ya mwani Zanzibar, Mkurugenzi Mtendaji Milele Zanzibar Foundation Khadija Shariff alieleza kuwa tatasi yake imeamua kutoa mchango wake kwa wakulima wa kilimo hicho kwa sababu zao hilo linalimwa na akinamama waliowengi.

“Dira yetu ni kuona akinamama wanainuka Kiuchumi na kuwa na mafanikio yaliobora kwa ajilia ya kujikombo na hali ya ngumu ya maisha” alieleza Bi Khadija.

Alifahamisha kuwa wameamua kufanya siku ya mwani maalumu kwa lengo la kulitangaza zao la mwani ndani na nje ya Nchi ili kuvutia wawekezaji kwa ajili ya kuwapatia soko wakulima wa zao hilo.

Akionekana kujibu maombi ya wakulima hao, Makamu wa Pili wa Rais, alisema kuwa maombi ya wakulima juu ukubwa wa kodi wanazotozwa wakulima hao anazichukuwa na kuahidi kuzingumza  katika ngazi za Serikali ili kuona kama waondoe au wapunguze kwa lengo la kuboresha maisha ya wakulima mwani.

“Lazima tuangalie namna gani ya kuwafanya wakulima wetu waweze kupata manufaa” alieleza Balozi.
Alieelza kuwa wanafanya hivyo kutokana na kufahamu Mchango mkubwa unaotokana na zao hilo licha ya changamoto zinazowakabili wakulima.

Alieleza kuwa watahakikisha Changamoto hizo zinafanyiwa kazi kwani tayari wamo katika mipango ya kuazisha viwanda vya kusarifia mwani kutokana na wadau mbali mbali ndani nan je ya nchi.

No comments:

Post a Comment

Pages