HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 16, 2017

NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO ATEMBELEA TEMESA

Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani katikati (aliyevaa suti) akimsikiliza Mkuu wa Kivuko/ Magogoni Kigamboni Mhandisi Lukombe King’ombe wakati akimpa taarifa ndani ya chumba cha kuongozea kivuko cha MV. KAZI alipotembelea kujionea utendaji kazi wake, wa kwanza kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu
Baadhi ya Wafanyakazi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Makao makuu wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Dk. Mussa Mgwatu wakati akisoma taarifa fupi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani aliyetembelea ofisi za wakala huo kujionea utendaji kazi na kusikiliza changamoto zinazoukabili wakala huo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu katikati akitoa ufafanuzi wakati alipokua akisoma taarifa ya wakala huo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani wa kwanza kushoto. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa wakala huo Hans Lyimo. Mheshimiwa Ngonyani alitembelea ofisi za wakala huo kujionea utendaji kazi na kusikiliza changamoto zinazoukabili wakala huo.
Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani katikati akimsikiliza Meneja wa Karakana ya Mt Depot Mhandisi Moses Humbe wa kwanza kushoto alipokua akimuelezea kuhusu utendaji kazi wa karakana hiyo. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu.
Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani (wa pili kulia) akishuka kutoka kwenye kivuko cha MV. KIGAMBONI mara baada ya kukagua utendaji kazi wake, kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu.
Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani katikati (aliyevaa suti) akipewa ufafanuzi kuhusu eneo panapojengwa chumba kipya cha kukatia tiketi eneo la Kigamboni na Mkuu wa Kivuko/ Magogoni Kigamboni Mhandisi Lukombe King’ombe (wa pili kushoto aliyenyoosha mkono). Wa pili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu anayesikiliza kwa makini.

No comments:

Post a Comment

Pages