HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 19, 2017

Mawakala wa benki ya CRDB watakiwa kuendeleza uadilifu

Mawakala wa benki ya CRDB kupitia huduma ya Fahari Huduma kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza, wakiwa kwenye semina iliyoyandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya kuwajengea weledi na uwezo wa kutoa huduma bora kwa wateja.

Mawakala kutoka wila ya za Nyamagana, Ilemela, Magu, Misungwi, Kwimba, Sengerema pamoja na Ukerewe walihudhuria kwenye semina hiyo iliyofanyika alhamisi iliyopita Oktoba 12,2017 Jijini Mwanza.

Akifungua semina hiyo, Mkurugenzi wa CRDB tawi la Nyanza Jijini Mwanza, Wambura Calystus aliwasihi mawakala hao kuwa waaminifu katika kuwahudumia wateja ikiwemo kutunza siri za mihamara ya pesa za wateja wao huku wakitoa huduma bora kama ilivyo ada ya benki ya CRDB wanayoiwakilisha katika maeneo yao.

Mawakala hao walieleza kwamba semina hiyo itawasaidia kuboresha huduma zao kwa wateja na hivyo kuwahimiza wateja wa benki ya CRDB kuendelea kutumia huduma za benki hiyo kwani zinapatikana kwa urahisi katika maeneo yote nchini.
Na Binagi Media Group
Mkurugenzi wa CRDB tawi la Nyanza Jijini Mwanza, Wambura Calystus, akifungua semina hiyo
Meneja wa CRDB tawi la Nyanza Jijini Mwanza, Mafwimbo Mulungu akizungumza kwenye semina hiyo
Afisa wa CRDB, Danford Muyango akiwasilisha mada kwenye semina hiyo
Mmoja wa maofisa wa benki ya CRDB, akizungumza kwenye semina hiyo
Afisa BIMA kutoka benki ya CRDB tawi la Nyanza, Jackline Jubilate akiwasilisha mada kwenye semina hiyo
Mmoja wa maofisa wa benki ya CRDB, akizungumza kwenye semina hiyo
Mmoja wa maofisa wa benki ya CRDB, akizungumza kwenye semina hiyo
Meneja biashara wa CRDB tawi la Nyanda, Eugenius Mashishanga (kushoto), akizungumza kwenye semina hiyo
Baadhi ya wakala wa CRDB wakichangia mada kwenye semina hiyo
Baadhi ya mawakala wa benki ya CRDB wakiwa kwenye semina hiyo.

No comments:

Post a Comment

Pages