HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 10, 2017

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC) LATOA MSAADA KWA WAGONJWA WA MOYO, WANAFUNZI SHULE YA MSINGI OLYMPIO

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Profesa Mohamed Janabi, akizungumza na uongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakati uongozi wa shirika hilo, ulipotembelea taasisi hiyo, Muhimbili Dar es Salaam, kuwaona wagonjwa na kutoa msaada wa fedha kwa watoto wawili kwa ajili kusaidia kufanyiwa upasuaji, ikiwa ni katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani, leo Oktoba 10, 2017.  Kushoto ni Kaimu Postamasta wa shirika hilo, Deo Kwiyukwa.
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deo Kwiyukwa, akizungumza na  Uongozi pamoja na Madaktari Bingwa wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, wakati uongozi wa shirika hilo, ulipotembelea taasisi hiyo, kuwaona wagonjwa na kutoa msaada wa fedha kwa watoto wawili wagonjwa wa moyo, kusaidia kufanyiwa upasuaji, ikiwa ni katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani leo Oktoba 10, 2017 jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Profesa Mohamed Janabi. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Profesa Mohamed Janabi (kulia), akimkabidhi kipeperushi cha taasisi hiyo, Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deo Kwiyukwa, wakati uongozi wa shirika hilo, ulipotembelea taasisi hiyo, kuwaona wagonjwa na kutoa msaada wa fedha kwa watoto wawili wagonjwa wa moyo, kusaidia kufanyiwa upasuaji, ikiwa ni katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani leo Oktoba 10, 2017 jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Profesa Mohamed Janabi, akizungumza na baadhi ya Maofisa wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakati wa ziara ya uongozi wa shirika katika taasisi hiyo, Dar es Salaam leo. Kulia ni Elia Madulesi na katikati ni Hassan Mwang'ombe.  
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deo Kwiyukwa (wa tatu kushoto), akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Profesa Mohamed Janabi (wa tatu kulia), mfano wa hundi ya sh. milioni 4 kwa ajili ya kusaidia matibabu ya watoto wawili wanaotarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo, wakati uongozi wa TPC, ulipotembelea taasisi hiyo katika kuadhimisha siku ya Posta Duniani, Dar es Salaam leo. Wa pili kulia ni Daktari bingwa wa upasuaji moyo watoto, Dkt. Godwin Sharau na wa kwanza ni Meneja Mkuu Usimamizi Biashara wa TPC, Hassan Mwang'ombe.

Daktari bingwa wa upasuaji moyo watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Dkt. Godwin Sharau (wa tano kulia), akiwapatia maelezo baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakati uongozi wa shirika ulipotembelea moja ya wodi za wagonjwa wa moyo kwenye taasisi hiyo leo jijini. Wa nne kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu wa shirika hilo, Deo Kwiyukwa. 
Daktari bingwa wa upasuaji moyo watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Dkt. Godwin Sharau (wa pili kushoto), akiwapatia maelezo baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakati uongozi wa shirika ulipotembelea moja ya wodi za wagonjwa wa moyo kwenye taasisi hiyo leo jijini katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani, Oktoba 10, 2017. Wa nne kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu wa shirika hilo, Deo Kwiyukwa.  
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deo Kwiyukwa, akiwa amembeba mtoto Delphina, ambaye ni mmoja wa watoto waliopatiwa msaada wa sh. milioni 2 kila mmoja na TPC kwa ajili ya matibabu ya upasuaji wa moyo, wakati uongozi wa shirika hilo, ulipotembelea kwenye wodi za wagonjwa wa moyo katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Muhimbili Dar es Salaam leo katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani. 
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deo Kwiyukwa, akifurai na mtoto Zainab Shabani (3), mmoja wa watoto waliopatiwa msaada wa sh. milioni 2 na TPC kwa ajili ya matibabu ya upasuaji wa moyo, wakati uongozi wa shirika hilo, ulipotembelea kwenye wodi za wagonjwa wa moyo katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Muhimbili Dar es Salaam leo katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani. Kulia ni mama yake, Fatuma Ahmad na kushoto, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa, Elia Madulesi. 
Daktari bingwa wa upasuaji moyo watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Dkt. Godwin Sharau (kulia), akiwaeleza jambo baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakati uongozi wa shirika hilo, ulipotembelea taasisi hiyo, kuwaona wagonjwa na kutoa msaada wa fedha kwa watoto wawili kusaidia kufanyiwa upasuaji ikiwa ni katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani leo Oktoba 10, 2017. Wa nne kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu wa shirika hilo, Deo Kwiyukwa.  
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deo Kwiyukwa, akizungumza na  waandishi wa habari, mara baada ya kumaliza ziara yao ya kutembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, leo jijini Dar es Salaam.
Daktari bingwa wa upasuaji moyo watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Dkt. Godwin Sharau (kulia), akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya uongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), ulipomaliza ziara yao kwenye taasisi hiyo, katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani, leo Oktoba 10, 2017. Wa pili kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu wa shirika hilo, Deo Kwiyukwa.  
Uongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), ukiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Madaktari bingwa wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, wakati ulipotembelea taasisi hiyo kuwaona wagonjwa na kutoa msaada katika kuadhimisha Siku ya Posta Duniani Dar es Salaam leo. 
Afisa Masoko wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Posta Kuu Dar es Salaam, James Msiani, akiwaeleza jambo wanafunzi wa Shule ya Msingi Olympio, walipotembelea Ofisi za Posta Kuu na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na posta, ikiwa ni katika maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Olympio, wakiwa na mwalimu wao, wakiwa katika Ofisi ya Posta Kuu kwa ajili kutembelea ofisi hizo, kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na posta, ikiwa ni katika maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani. Wa pili kushoto ni Afisa Masoko wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Posta Kuu Dar es Salaam, James Msiani.

No comments:

Post a Comment

Pages