HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 23, 2018

MAKAMU WA RAIS AWATAKA MAKAMBA, MAKONDA KUDHIBITI MAFURIKO

NA JANETH JOVIN

MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan amemtaka Waziri wa  Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, January Makamba na Mkuu wa Mkoa wa  Dar es Salaam Paul Makonda kuchukua hatua za haraka katika kukabiliana na tatizo la mafuriko na uharibifu wa mazingira katika jiji hilo.

Mama Samia amewataka viongozi hao kuunda kamati maalum ya kushughulikia matatizo hayo haraka iwezekanavyo.

Makamu ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akiongoza mkutano wa wadau wa mazingira kuhusu changamoto ya mafuriko na hifadhi ya mazingira katika jiji hilo.
Alisema kwa muda mrefu kumekuwa hakuna umakini katika kusimamia masuala ya mazingira nchini licha kuwepo kwa sheria mbalimbali.

"Mambo mengi na hasara zinazotekea wakati wa mafuriko zinasababishwa na sisi wenyewe watu wamekuwa hawana utamaduni wa kuyatunza mazingira yao sasa natoa maagizo hiundwe kamati ya mazingira haraka ambayo itapokea miradi yote ya kila wilaya na kuangalia ipi itatekelezeka.

Kamati hii itakaoundwa haina haja ya fedha na nisije nikasikia kuwa imeshindwa kufanya kazi kutokana na kukosa na fedha kwani ni sehemu ya majukumu yao ya kazi"alisema
Aidha alisema kuna uhitaji wa kutolewa elimu ya mazingira kwa jamii na kupeana taarifa mbalimbali zinazohusiana na mazingira. 

Naye Waziri Makamba alisema ni wakati wa kutafakari na kupata jawabu la kudumu la suala la mafuriko yanayotokea katika jiji la Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages